< Zaburi 29 >

1 Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
天主的眾子,請讚美上主,請將讚美光榮,歸於上主。
2 Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
請將主的榮耀,歸於上主,穿上聖潔華服,朝拜上主。
3 Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
上主的聲音響徹水面,天主雷鳴在顯示莊嚴,上主臨到澎湃的水面。
4 Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
上主的聲音具有威權,上主的聲音具有莊嚴。
5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
上主的聲音劈斷香柏,上主折斷黎巴嫩香柏;
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
使黎巴嫩像牛犢一樣舞蹈,使息爾翁像小牛一樣跳躍。
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
上主的聲音放射出火舌。
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
上主的聲音震動了曠野,上主震動了卡士德曠野。
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
上主的聲音搖撼橡樹,剝光森林;凡在祂殿中的都齊聲高呼:光榮。
10 Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
上主坐在洪水之上,上主永遠高坐為王。
11 Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.
上主必將勇力賜給祂的百姓,上主必以平安祝福祂的人民。

< Zaburi 29 >