< Zaburi 28 >

1 Yahwe, ninalia; mwamba wangu, usinipuuze. Ikiwa haunijibu, nitaungana na wale waendao chini kaburini.
De David. C’est vers toi, Yahweh, que je crie; mon rocher, ne reste pas sourd à ma voix, de peur que, si tu gardes le silence, je ne ressemble à ceux qui descendent dans la fosse.
2 Sikia kilio cha kusihi kwangu pale niitapo msaada kutoka kwako, niinuapo mikono yangu mbele ya mahali patakatifu zaidi!
Ecoute la voix de mes supplications, quand je crie vers toi, quand j’élève mes mains vers ton saint sanctuaire.
3 Usiniburute pamoja na waovu, wale wafanyao uovu, waongeao amani na majirani zao lakini mioyoni mwao mna uovu.
Ne m’emporte pas avec les méchants et les artisans d’iniquité, qui parlent de paix à leur prochain, et qui ont la malice dans le cœur.
4 Uwape kulingana na sitahili ya matendo yao na uwalipe kulingana na madai ya maovu yao, uwalipe kwa ajili ya kazi ya mikono yao na uwape kile wanachostahili.
Rends-leur selon leurs œuvres, et selon la malice de leurs actions; rends-leur selon l’ouvrage de leurs mains, donne-leur le salaire qu’ils méritent.
5 Kwa sababu hawayaelewi matendo ya Yahwe wala kazi ya mikono yake, atawakanyaga kanyaga chini na hata wajenga tena wao.
Car ils ne prennent pas garde aux œuvres de Yahweh, à l’ouvrage de ses mains: il les détruira et ne les bâtira pas.
6 Abarikiwe Yahwe kwa sababu yeye amesikia sauti ya kusihi kwangu!
Béni soit Yahweh, car il a entendu la voix de mes supplications!
7 Yahwe ni nguvu yangu na ngao yangu; moyo wangu wa humwamini yeye, na ninasaidiwa. Kwa hiyo moyo wangu hufurahia sana, nami nitamsifu yeye kwa kuimba.
Yahweh est ma force et mon bouclier; en lui s’est confié mon cœur. J’ai été secouru; aussi mon cœur est dans l’allégresse, et je le louerai par mes cantiques.
8 Yahwe ni nguvu ya watu wake, naye ni mkombozi salama wa wapakwa mafuta wake.
Yahweh est la force de son peuple, il est une forteresse de salut pour son Oint.
9 Uwaokoe watu wako na uwabariki warithi wako. Uwe mchungaji wao na uwabebe milele.
Sauve ton peuple et bénis ton héritage! Sois leur pasteur et porte-les à jamais!

< Zaburi 28 >