< Zaburi 27 >

1 Yahwe ni nuru yangu na wokovu wangu; nimuogope nani? Yahwe ni salama ya maisha yangu; ni mhofu nani?
Господь просвещение мое и спаситель мой, кого убоюся? Господь защититель живота моего, от кого устрашуся?
2 Wakati waovu waliponijia kunila mwili wangu, wapinzani wangu na adui zangu walijikwaa na wakaanguka.
Внегда приближатися на мя злобующым, еже снести плоти моя, оскорбляющии мя и врази мои, тии изнемогоша и падоша.
3 Ingawa jeshi hujipanga kupigana na mimi, moyo wangu hautaogopa; japo vita vijapo inuka kupigana nami hata hapo nitabaki kuwa jasiri.
Аще ополчится на мя полк, не убоится сердце мое: аще востанет на мя брань, на него аз уповаю.
4 Kitu kimoja nimekiomba kwa Yahwe, nami nitakitafuta hicho: kwamba niweze kukaa katika nyumba ya Yahwe siku zote za maisha yangu, kuutazama uzuri wa Yahwe na kutafakari hekaruni mwake.
Едино просих от Господа, то взыщу: еже жити ми в дому Господни вся дни живота моего, зрети ми красоту Господню и посещати храм Святый Его.
5 Kwa kuwa katika siku ya shida atanificha nyumbani mwake; atanificha katika mfuniko wa hema lake. Yeye ataniinua juu ya mwamba!
Яко скры мя в селении Своем в день зол моих, покры мя в тайне селения Своего, на камень вознесе мя.
6 Kisha kichwa changu kitainuliwa juu ya maadui wote wanizungukao, nami nitatoa sadaka ya furaha hemani mwake! Nitaimba na kutunga nyimbo kwa Yahwe!
И ныне се, вознесе главу мою на враги моя: обыдох и пожрох в селении Его жертву хваления и воскликновения: пою и воспою Господеви.
7 Sikia, sauti yangu nikuitapo, Yahwe! Unihurumie, na unijibu!
Услыши, Господи, глас мой, имже воззвах, помилуй мя и услыши мя.
8 Moyo wangu huongea kuhusu wewe, “Utafute uso wake!” Nami nautafuta uso wako, Yahwe!
Тебе рече сердце мое: Господа взыщу, взыска Тебе лице мое, лица Твоего, Господи, взыщу.
9 Usiufiche uso wako mbali na mimi; usinikasirikie mimi mtumishi wako! Wewe umekuwa msaada wangu; usiniache wala kunitelekeza, Mungu wa wokovu wangu!
Не отврати лица Твоего от мене и не уклонися гневом от раба Твоего: помощник мой буди, не отрини мене и не остави мене, Боже, Спасителю мой.
10 Hata kama baba yangu na mama yangu wakiniacha, Yahwe utanitunza kwako.
Яко отец мой и мати моя остависта мя, Господь же восприят мя.
11 Unifundishe njia yako, Yahwe! Kwa sababu ya adui zangu uniongoze katika njia salama.
Законоположи ми, Господи, в пути Твоем, и настави мя на стезю правую враг моих ради.
12 Usiwaache adui zangu wanifanyie watamanivyo, kwa sababu mashahidi wa uongo wameinuka kinyume namimi, nao wanapumua vurugu!
Не предаждь мене в душы стужающих ми: яко восташа на мя свидетеле неправеднии, и солга неправда себе.
13 Kitu gani kingeweza kunitokea kama nisingeamini kuwa nitauona uzuri wa Yahwe katika nchi ya walio hai?
Верую видети благая Господня на земли живых.
14 Umngoje Yahwe; uwe imara, na moyo wako uwe jasiri! Umngoje Yahwe!
Потерпи Господа, мужайся, и да крепится сердце твое, и потерпи Господа.

< Zaburi 27 >