< Zaburi 27 >

1 Yahwe ni nuru yangu na wokovu wangu; nimuogope nani? Yahwe ni salama ya maisha yangu; ni mhofu nani?
مزمور داوود. خداوند نور و نجات من است، از که بترسم؟ خداوند حافظ جان من است از که هراسان شوم؟
2 Wakati waovu waliponijia kunila mwili wangu, wapinzani wangu na adui zangu walijikwaa na wakaanguka.
هنگامی که بدکاران بر من هجوم آوردند تا مرا نابود کنند، لغزیدند و افتادند.
3 Ingawa jeshi hujipanga kupigana na mimi, moyo wangu hautaogopa; japo vita vijapo inuka kupigana nami hata hapo nitabaki kuwa jasiri.
حتی اگر لشکری بر ضد من برخیزد، ترسی به دل راه نخواهم داد! اگر علیه من جنگ بر پا کنند، به خدا توکل خواهم کرد و نخواهم ترسید!
4 Kitu kimoja nimekiomba kwa Yahwe, nami nitakitafuta hicho: kwamba niweze kukaa katika nyumba ya Yahwe siku zote za maisha yangu, kuutazama uzuri wa Yahwe na kutafakari hekaruni mwake.
تنها خواهش من از خداوند این است که اجازه دهد تمام روزهای عمرم در حضور او زیست کنم و در خانهٔ او به او تفکر نمایم و جمال او را مشاهده کنم.
5 Kwa kuwa katika siku ya shida atanificha nyumbani mwake; atanificha katika mfuniko wa hema lake. Yeye ataniinua juu ya mwamba!
در روزهای سخت زندگی، او مرا در خانهٔ خود پناه خواهد داد، مرا حفظ خواهد کرد و بر صخره‌ای بلند و مطمئن استوار خواهد ساخت.
6 Kisha kichwa changu kitainuliwa juu ya maadui wote wanizungukao, nami nitatoa sadaka ya furaha hemani mwake! Nitaimba na kutunga nyimbo kwa Yahwe!
آنگاه بر دشمنانی که مرا احاطه کرده‌اند پیروز خواهم شد؛ با فریاد شادی در خیمهٔ او قربانیها تقدیم خواهم نمود و برای خداوند سرود شکرگزاری خواهم خواند.
7 Sikia, sauti yangu nikuitapo, Yahwe! Unihurumie, na unijibu!
ای خداوند، فریاد مرا بشنو و رحمت فرموده، دعایم را اجابت کن.
8 Moyo wangu huongea kuhusu wewe, “Utafute uso wake!” Nami nautafuta uso wako, Yahwe!
تو گفته‌ای که تو را بطلبم، من نیز از ته دل می‌گویم که ای خداوند تو را خواهم طلبید.
9 Usiufiche uso wako mbali na mimi; usinikasirikie mimi mtumishi wako! Wewe umekuwa msaada wangu; usiniache wala kunitelekeza, Mungu wa wokovu wangu!
خود را از من پنهان نکن؛ بر من خشمگین مشو و مرا از حضورت نران. تو مددکار من بوده‌ای، مرا طرد نکن؛ ای خدای نجا‌ت‌دهندۀ من، مرا ترک نکن!
10 Hata kama baba yangu na mama yangu wakiniacha, Yahwe utanitunza kwako.
حتی اگر پدر و مادرم مرا از خود برانند، خداوند مرا نزد خود خواهد پذیرفت.
11 Unifundishe njia yako, Yahwe! Kwa sababu ya adui zangu uniongoze katika njia salama.
ای خداوند، مرا به راه راست خود هدایت کن تا از گزند دشمن در امان باشم.
12 Usiwaache adui zangu wanifanyie watamanivyo, kwa sababu mashahidi wa uongo wameinuka kinyume namimi, nao wanapumua vurugu!
مرا به دست بدخواهانم نسپار، زیرا این ظالمان می‌خواهند با شهادت دروغ خود، بر ضد من قیام کنند.
13 Kitu gani kingeweza kunitokea kama nisingeamini kuwa nitauona uzuri wa Yahwe katika nchi ya walio hai?
به یقین باور دارم که نیکویی خداوند را بار دیگر در این دنیا، در دیار زندگان خواهم دید.
14 Umngoje Yahwe; uwe imara, na moyo wako uwe jasiri! Umngoje Yahwe!
به خداوند امیدوار باش و بر او توکل کن. ایمان داشته باش و ناامید نشو.

< Zaburi 27 >