< Zaburi 27 >

1 Yahwe ni nuru yangu na wokovu wangu; nimuogope nani? Yahwe ni salama ya maisha yangu; ni mhofu nani?
“Of David.” The Lord is my light and my salvation; of whom shall I be afraid? the Lord is the fortress of my life; of whom shall I have dread?
2 Wakati waovu waliponijia kunila mwili wangu, wapinzani wangu na adui zangu walijikwaa na wakaanguka.
When evil-doers come near against me to eat up my flesh, my assailants and my enemies at me: then do they stumble and fall.
3 Ingawa jeshi hujipanga kupigana na mimi, moyo wangu hautaogopa; japo vita vijapo inuka kupigana nami hata hapo nitabaki kuwa jasiri.
If an army should encamp against me, my heart shall not fear: if war should arise against me, even then will I have trust.
4 Kitu kimoja nimekiomba kwa Yahwe, nami nitakitafuta hicho: kwamba niweze kukaa katika nyumba ya Yahwe siku zote za maisha yangu, kuutazama uzuri wa Yahwe na kutafakari hekaruni mwake.
One thing have I asked of the Lord, that I will seek for: that I may dwell in the house of the Lord all the days of my life, to behold the loveliness of the Lord, and to be every morning early in his temple.
5 Kwa kuwa katika siku ya shida atanificha nyumbani mwake; atanificha katika mfuniko wa hema lake. Yeye ataniinua juu ya mwamba!
For he will hide me in his pavilion on the day of evil; he will conceal me in the secret of his tabernacle; upon a rock will he place me high.
6 Kisha kichwa changu kitainuliwa juu ya maadui wote wanizungukao, nami nitatoa sadaka ya furaha hemani mwake! Nitaimba na kutunga nyimbo kwa Yahwe!
And now will my head be lifted up above my enemies all round about me; and I will sacrifice in his tabernacle sacrifices of joy: I will sing, and I will triumphantly play unto the Lord.
7 Sikia, sauti yangu nikuitapo, Yahwe! Unihurumie, na unijibu!
Hear, O Lord, my voice, [when] I call, and be gracious unto me, and answer me.
8 Moyo wangu huongea kuhusu wewe, “Utafute uso wake!” Nami nautafuta uso wako, Yahwe!
Of thee, said my heart, “Seek ye my presence”: thy presence, Lord, will I seek.
9 Usiufiche uso wako mbali na mimi; usinikasirikie mimi mtumishi wako! Wewe umekuwa msaada wangu; usiniache wala kunitelekeza, Mungu wa wokovu wangu!
Hide [then] not thy face from me; reject not in anger thy servant, thou [who] hast been my help: cast me not off, nor forsake me, O God of my salvation.
10 Hata kama baba yangu na mama yangu wakiniacha, Yahwe utanitunza kwako.
For my father and my mother have forsaken me; but the Lord will take me up.
11 Unifundishe njia yako, Yahwe! Kwa sababu ya adui zangu uniongoze katika njia salama.
Point me out thy way, O Lord! and guide me on a level path, because of those that regard me enviously.
12 Usiwaache adui zangu wanifanyie watamanivyo, kwa sababu mashahidi wa uongo wameinuka kinyume namimi, nao wanapumua vurugu!
Give me not up to the [revengeful] desire of my assailants; for there are risen up against me false witnesses, and such as utter violence.
13 Kitu gani kingeweza kunitokea kama nisingeamini kuwa nitauona uzuri wa Yahwe katika nchi ya walio hai?
Unless I had believed to see the goodness of the Lord in the land of life—
14 Umngoje Yahwe; uwe imara, na moyo wako uwe jasiri! Umngoje Yahwe!
Wait on the Lord; be strong, and let thy heart be of good courage; and only wait on the Lord.

< Zaburi 27 >