< Zaburi 26 >

1 Unihukumu mimi, Yahwe, kwa kuwa nimeenenda katika uadilifu; nimeamini katika Yahwe bila kusita.
Defiéndeme, oh Yavé, porque en mi integridad anduve, Y en Yavé confié sin titubear.
2 Unichunguze, Yahwe, na unijaribu; uujaribu usafi wa sehemu zangu za ndani na moyoni mwangu!
Examíname, oh Yavé, y pruébame. Escudriña lo más íntimo de mi personalidad y mi corazón,
3 Kwa maana uaminifu wa agano lako uko mbele ya macho yangu, na mwenendo wangu ni katika uaminifu wako.
Porque tu misericordia está delante de mis ojos Y ando en tu verdad.
4 Mimi sichangamani na watu waovu, wala sichangamani na watu wanafiki.
No me siento con hombres falsos Ni ando con hipócritas.
5 Ninachukia waovu, na siishi na waovu.
Aborrezco la reunión de perversos Y no me sentaré con los inicuos.
6 Ninaosha mikono yangu kounesha sina hatia, na kuikaribia madhabahu yako, Yahwe,
Lavaré en inocencia mis manos, Y así andaré en torno a tu altar, oh Yavé,
7 kuimba wimbo wa sauti ya sifa na kutoa taarifa ya matendo yako yote ya ajabu.
Para hacer resonar mi voz de gratitud Y contar todas tus maravillas.
8 Yahwe, ninaipenda nyumba ninayoishi, mahali ambapo utukufu wako unaishi!
Oh Yavé, yo amo la Casa donde moras, Y el lugar donde reside tu gloria.
9 Usiniangamize pamoja na wenye dhambi, au maisha yangu na watu wenye kiu ya kumwaga damu,
No arrebates mi alma con los pecadores, Ni mi vida con hombres sanguinarios,
10 ambao katika mikono yao kuna njama, na ambao mkono wa kuume umejaa rushwa.
En las manos de los cuales está el crimen, Cuya mano derecha está llena de sobornos.
11 Lakini kwangu mimi, nitaenenda katika uadilifu; uniokoe na unihurumie.
En cuanto a mí, andaré en mi integridad. ¡Redímeme y ten misericordia de mí!
12 Miguu yangu husimama sehemu salama; katika kusanyiko la watu nitambariki Yahwe!
Mis pies están en suelo firme. Bendeciré a Yavé en las congregaciones.

< Zaburi 26 >