< Zaburi 26 >
1 Unihukumu mimi, Yahwe, kwa kuwa nimeenenda katika uadilifu; nimeamini katika Yahwe bila kusita.
In finem, Psalmus David. Iudica me Domine, quoniam ego in innocentia mea ingressus sum: et in Domino sperans non infirmabor.
2 Unichunguze, Yahwe, na unijaribu; uujaribu usafi wa sehemu zangu za ndani na moyoni mwangu!
Proba me Domine, et tenta me: ure renes meos et cor meum.
3 Kwa maana uaminifu wa agano lako uko mbele ya macho yangu, na mwenendo wangu ni katika uaminifu wako.
Quoniam misericordia tua ante oculos meos est: et complacui in veritate tua.
4 Mimi sichangamani na watu waovu, wala sichangamani na watu wanafiki.
Non sedi cum concilio vanitatis: et cum iniqua gerentibus non introibo.
5 Ninachukia waovu, na siishi na waovu.
Odivi ecclesiam malignantium: et cum impiis non sedebo.
6 Ninaosha mikono yangu kounesha sina hatia, na kuikaribia madhabahu yako, Yahwe,
Lavabo inter innocentes manus meas: et circumdabo altare tuum Domine:
7 kuimba wimbo wa sauti ya sifa na kutoa taarifa ya matendo yako yote ya ajabu.
Ut audiam vocem laudis, et enarrem universa mirabilia tua.
8 Yahwe, ninaipenda nyumba ninayoishi, mahali ambapo utukufu wako unaishi!
Domine dilexi decorem domus tuæ, et locum habitationis gloriæ tuæ.
9 Usiniangamize pamoja na wenye dhambi, au maisha yangu na watu wenye kiu ya kumwaga damu,
Ne perdas cum impiis Deus animam meam, et cum viris sanguinum vitam meam:
10 ambao katika mikono yao kuna njama, na ambao mkono wa kuume umejaa rushwa.
In quorum manibus iniquitates sunt: dextera eorum repleta est muneribus.
11 Lakini kwangu mimi, nitaenenda katika uadilifu; uniokoe na unihurumie.
Ego autem in innocentia mea ingressus sum: redime me, et miserere mei.
12 Miguu yangu husimama sehemu salama; katika kusanyiko la watu nitambariki Yahwe!
Pes meus stetit in directo: in ecclesiis benedicam te Domine.