< Zaburi 26 >

1 Unihukumu mimi, Yahwe, kwa kuwa nimeenenda katika uadilifu; nimeamini katika Yahwe bila kusita.
(다윗의 시) 내가 나의 완전함에 행하였사오며 요동치 아니하고 여호와를 의지하였사오니 여호와여, 나를 판단하소서
2 Unichunguze, Yahwe, na unijaribu; uujaribu usafi wa sehemu zangu za ndani na moyoni mwangu!
여호와여, 나를 살피시고 시험하사 내 뜻과 내 마음을 단련하소서
3 Kwa maana uaminifu wa agano lako uko mbele ya macho yangu, na mwenendo wangu ni katika uaminifu wako.
주의 인자하심이 내 목전에 있나이다 내가 주의 진리 중에 행하여
4 Mimi sichangamani na watu waovu, wala sichangamani na watu wanafiki.
허망한 사람과 같이 앉지 아니하였사오니 간사한 자와 동행치도 아니하리이다
5 Ninachukia waovu, na siishi na waovu.
내가 행악자의 집회를 미워하오니 악한 자와 같이 앉지 아니하리이다
6 Ninaosha mikono yangu kounesha sina hatia, na kuikaribia madhabahu yako, Yahwe,
여호와여, 내가 무죄하므로 손을 씻고 주의 단에 두루 다니며
7 kuimba wimbo wa sauti ya sifa na kutoa taarifa ya matendo yako yote ya ajabu.
감사의 소리를 들리고 주의 기이한 모든 일을 이르리이다
8 Yahwe, ninaipenda nyumba ninayoishi, mahali ambapo utukufu wako unaishi!
여호와여, 내가 주의 계신 집과 주의 영광이 거하는 곳을 사랑하오니
9 Usiniangamize pamoja na wenye dhambi, au maisha yangu na watu wenye kiu ya kumwaga damu,
내 영혼을 죄인과 함께 내 생명을 살인자와 함께 거두지 마소서
10 ambao katika mikono yao kuna njama, na ambao mkono wa kuume umejaa rushwa.
저희 손에 악특함이 있고 그 오른손에 뇌물이 가득하오나
11 Lakini kwangu mimi, nitaenenda katika uadilifu; uniokoe na unihurumie.
나는 나의 완전함에 행하오리니 나를 구속하시고 긍휼히 여기소서
12 Miguu yangu husimama sehemu salama; katika kusanyiko la watu nitambariki Yahwe!
내 발이 평탄한 데 섰사오니 회중에서 여호와를 송축하리이다

< Zaburi 26 >