< Zaburi 26 >

1 Unihukumu mimi, Yahwe, kwa kuwa nimeenenda katika uadilifu; nimeamini katika Yahwe bila kusita.
BY DAVID. Judge me, O YHWH, for I have walked in my integrity, And I have trusted in YHWH, I do not slide.
2 Unichunguze, Yahwe, na unijaribu; uujaribu usafi wa sehemu zangu za ndani na moyoni mwangu!
Try me, O YHWH, and prove me, My reins and my heart [are] purified,
3 Kwa maana uaminifu wa agano lako uko mbele ya macho yangu, na mwenendo wangu ni katika uaminifu wako.
For Your kindness [is] before my eyes, And I have habitually walked in Your truth.
4 Mimi sichangamani na watu waovu, wala sichangamani na watu wanafiki.
I have not sat with vain men, And I do not enter with pretenders.
5 Ninachukia waovu, na siishi na waovu.
I have hated the assembly of evildoers, And I do not sit with the wicked.
6 Ninaosha mikono yangu kounesha sina hatia, na kuikaribia madhabahu yako, Yahwe,
I wash my hands in innocence, And I go around Your altar, O YHWH.
7 kuimba wimbo wa sauti ya sifa na kutoa taarifa ya matendo yako yote ya ajabu.
To sound with a voice of confession, And to recount all Your wonders.
8 Yahwe, ninaipenda nyumba ninayoishi, mahali ambapo utukufu wako unaishi!
YHWH, I have loved the habitation of Your house, And the place of the Dwelling Place of Your glory.
9 Usiniangamize pamoja na wenye dhambi, au maisha yangu na watu wenye kiu ya kumwaga damu,
Do not gather my soul with sinners, And my life with men of blood,
10 ambao katika mikono yao kuna njama, na ambao mkono wa kuume umejaa rushwa.
In whose hand [is] a wicked scheme, And their right hand [is] full of bribes.
11 Lakini kwangu mimi, nitaenenda katika uadilifu; uniokoe na unihurumie.
And I walk in my integrity, Redeem me, and favor me.
12 Miguu yangu husimama sehemu salama; katika kusanyiko la watu nitambariki Yahwe!
My foot has stood in uprightness, In assemblies I bless YHWH!

< Zaburi 26 >