< Zaburi 25 >
1 Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
К Тебе, Господи, воздвигох душу мою, Боже мой, на Тя уповах, да не постыжуся во век, ниже да посмеютмися врази мои:
2 Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
ибо вси терпящии Тя не постыдятся.
3 Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
Да постыдятся беззаконнующии вотще.
4 Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
Пути Твоя, Господи, скажи ми и стезям Твоим научи мя.
5 Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
Настави мя на истину Твою и научи мя: яко Ты еси Бог спас мой, и Тебе терпех весь день.
6 Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
Помяни щедроты Твоя, Господи, и милости Твоя, яко от века суть.
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
Грех юности моея и неведения моего не помяни: по милости Твоей помяни мя Ты, ради благости Твоея, Господи.
8 Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
Благ и прав Господь, сего ради законоположит согрешающым на пути.
9 Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
Наставит кроткия на суд, научит кроткия путем Своим.
10 Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
Вси путие Господни милость и истина, взыскающым завета Его и свидения Его.
11 Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
Ради имене Твоего, Господи, и очести грех мой, мног бо есть.
12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
Кто есть человек бояйся Господа? Законоположит ему на пути, егоже изволи.
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
Душа его во благих водворится, и семя его наследит землю.
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
Держава Господь боящихся Его, и завет Его явит им.
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
Очи мои выну ко Господу, яко Той исторгнет от сети нозе мои.
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
Призри на мя и помилуй мя, яко единород и нищь есмь аз.
17 Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
Скорби сердца моего умножишася, от нужд моих изведи мя.
18 Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
Виждь смирение мое и труд мой, и остави вся грехи моя.
19 Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
Виждь враги моя, яко умножишася, и ненавидением неправедным возненавидеша мя.
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
Сохрани душу мою и избави мя, да не постыжуся, яко уповах на Тя.
21 Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
Незлобивии и правии прилепляхуся мне, яко потерпех Тя, Господи.
22 Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!
Избави, Боже, Израиля от всех скорбей его.