< Zaburi 25 >

1 Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
psalmus David ad te Domine levavi animam meam
2 Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
Deus meus in te confido non erubescam
3 Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
neque inrideant me inimici mei etenim universi qui sustinent te non confundentur
4 Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
confundantur omnes iniqua agentes supervacue vias tuas Domine demonstra mihi et semitas tuas doce me
5 Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
dirige me in veritatem tuam et doce me quoniam tu es Deus salvator meus et te sustinui tota die
6 Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
reminiscere miserationum tuarum Domine et misericordiarum tuarum quia a saeculo sunt
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
delicta iuventutis meae et ignorantias meas ne memineris secundum misericordiam tuam memento mei tu; propter bonitatem tuam Domine
8 Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
dulcis et rectus Dominus propter hoc legem dabit delinquentibus in via
9 Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
diriget mansuetos in iudicio docebit mites vias suas
10 Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
universae viae Domini misericordia et veritas requirentibus testamentum eius et testimonia eius
11 Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
propter nomen tuum Domine et propitiaberis peccato meo multum est enim
12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
quis est homo qui timet Dominum legem statuet ei in via quam elegit
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
anima eius in bonis demorabitur et semen ipsius hereditabit terram
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
firmamentum est Dominus timentibus eum et testamentum ipsius ut manifestetur illis
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
oculi mei semper ad Dominum quoniam ipse evellet de laqueo pedes meos
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
respice in me et miserere mei quia unicus et pauper sum ego
17 Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
tribulationes cordis mei multiplicatae sunt de necessitatibus meis erue me
18 Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
vide humilitatem meam et laborem meum et dimitte universa delicta mea
19 Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
respice inimicos meos quoniam multiplicati sunt et odio iniquo oderunt me
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
custodi animam meam et erue me non erubescam quoniam speravi in te
21 Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
innocentes et recti adheserunt mihi quia sustinui te
22 Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!
libera Deus Israhel ex omnibus tribulationibus suis

< Zaburi 25 >