< Zaburi 25 >
1 Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
Psaume de David. ALEPH. Vers toi, Yahweh, j’élève mon âme, mon Dieu.
2 Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
En toi je me confie: que je n’aie pas de confusion! Que mes ennemis ne se réjouissent pas à mon sujet!
3 Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
Non, aucun de ceux qui espèrent en toi ne sera confondu; ceux là seront confondus qui sont infidèles sans cause.
4 Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
Yahweh, fais-moi connaître tes voies, enseigne-moi tes sentiers.
5 Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
Conduis-moi dans ta vérité, VAV. et instruis-moi, car tu es le Dieu de mon salut; tout le jour en toi j’espère.
6 Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
Souviens-toi de ta miséricorde, Yahweh, et de ta bonté car elles sont éternelles.
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
Ne te souviens pas des péchés de ma jeunesse ni de mes transgressions; souviens-toi de moi selon ta miséricorde, à cause de ta bonté, ô Yahweh,
8 Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
Yahweh est bon et droit; c’est pourquoi il indique aux pécheurs la voie.
9 Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
Il fait marcher les humbles dans la justice, il enseigne aux humbles sa voie.
10 Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
Tous les sentiers de Yahweh sont miséricorde et fidélité, pour ceux qui gardent son alliance et ses commandements.
11 Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
A cause de ton nom, Yahweh, tu pardonneras mon iniquité, car elle est grande.
12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
Quel est l’homme qui craint Yahweh? Yahweh lui montre la voie qu’il doit choisir.
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
Son âme repose dans le bonheur, et sa postérité possédera le pays.
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
La familiarité de Yahweh est pour ceux qui le craignent; il leur fait connaître les bénédictions de son alliance.
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
J’ai les yeux constamment tournés vers Yahweh, car c’est lui qui tirera mes pieds du lacet.
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
Regarde-moi et prends pitié de moi, car je suis délaissé et malheureux.
17 Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
Les angoisses de mon cœur se sont accrues: tire-moi de ma détresse!
18 Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
Vois ma misère et ma peine, et pardonne tous mes péchés.
19 Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
Vois combien sont nombreux mes ennemis, et quelle haine violente ils ont contre moi!
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
Garde mon âme et sauve-moi! Que je ne sois pas confus, car j’ai mis en toi ma confiance!
21 Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
Que l’innocence et la droiture me protègent, car j’espère en toi.
22 Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!
O Dieu, délivre Israël de toutes ses angoisses!