< Zaburi 25 >
1 Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
A psalm of David. To you, O Lord, I lift up my heart: all the day I wait for you.
2 Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
In you I trust, put me not to shame; let not my foes exult over me.
3 Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
None will be shamed who wait for you, but shame will fall upon wanton traitors.
4 Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
Make me, O Lord, to know your ways: teach me your paths.
5 Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
In your faithfulness guide me and teach me, for you are my God and my saviour.
6 Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
Remember your pity, O Lord, and your kindness, for they have been ever of old.
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
Do not remember the sins of my youth; remember me in kindness, because of your goodness, Lord.
8 Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
Good is the Lord and upright, so he teaches sinners the way.
9 Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
The humble he guides in the right, he teaches the humble his way.
10 Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
All his ways are loving and loyal to those who observe his charges and covenant.
11 Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
Be true to your name Lord, forgive my many sins.
12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
Who then is the person who fears the Lord? He will teach them the way to choose.
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
They will live in prosperity, their children will inherit the land.
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
The Lord gives guidance to those who fear him, and with his covenant he makes them acquainted.
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
My eyes are ever toward the Lord, for out of the net he brings my foot.
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
Turn to me with your favour, for I am lonely and crushed
17 Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
In my heart are strain and storm; bring me out of my distresses.
18 Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
Look on my misery and trouble, and pardon all my sins,
19 Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
look on my foes oh, so many! And their cruel hatred towards me.
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
Deliver me, keep me, and shame not one who takes refuge in you.
21 Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
May integrity and innocence preserve me, for I wait for you, O Lord.
22 Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!
Redeem Israel, O God, from all its distresses.