< Zaburi 25 >
1 Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
א To you, Adonai, do I lift up my soul.
2 Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
בּ My God, I have trusted in you. Don’t let me be shamed. Don’t let my enemies triumph over me.
3 Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
גּ Yes, no one who waits for you shall be shamed. They shall be shamed who deal treacherously without cause.
4 Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
דּ Show me your ways, Adonai. Teach me your paths.
5 Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
ה Guide me in your truth, and teach me, For you are the God of my yesha' ·salvation·, I wait for you all day long.
6 Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
ז Adonai, remember your tender rachamim ·merciful loves· and your chesed ·loving-kindness·, for they are from old times.
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
ח Don’t remember the habitual sins ·missing the marks· of my youth, nor my rebellious breaches of relationships. Remember me according to your chesed ·loving-kindness·, for your goodness’ sake, Adonai.
8 Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
ט Good and upright is Adonai, therefore he will instruct people who sin ·intentionally miss the mark goal· in the way.
9 Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
י He will guide the humble in mishpat ·justice·. He will teach the humble his way.
10 Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
כּ All the paths of Adonai are chesed ·loving-kindness· and truth to such as keep his covenant and his testimonies.
11 Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
ל For your name’s sake, Adonai, pardon my depravity (moral evil), for it is great.
12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
מ What man is he who fears Adonai? He shall instruct him in the way that he shall choose.
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
נ His soul shall dwell at ease. His offspring shall inherit the land.
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
ס The friendship of Adonai is with those who fear him. He will show them his covenant.
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
ע My eyes are ever on Adonai, for he will pluck my feet out of the net.
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
פ Turn to me, and have mercy on me, for I am desolate and afflicted.
17 Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
צ The troubles of my heart are enlarged. Oh bring me out of my distresses.
18 Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
ר Consider my affliction and my travail. Forgive all my habitual sins ·missing the marks·.
19 Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
ר Consider my enemies, for they are many. They hate me with cruel hatred.
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
שׁ Oh keep my soul, and deliver me. Let me not be disappointed, for I take refuge in you.
21 Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
תּ Let integrity and uprightness preserve me, for I wait for you.
22 Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!
Redeem Israel [God prevails], God, out all of his troubles.