< Zaburi 25 >

1 Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
“A psalm of David.” To thee, O LORD! do I lift up my soul.
2 Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
O my God! I trust in thee; let me not be put to shame! Let not my enemies triumph over me!
3 Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
Yea, none that hope in thee shall be put to shame: They shall be put to shame who wickedly forsake thee.
4 Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
Cause me to know thy ways, O LORD! Teach me thy paths!
5 Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
Lead me in thy truth, and teach me! For thou art the God from whom cometh my help; In thee do I trust at all times!
6 Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
Remember thy loving-kindness, O LORD! and thy tender mercy, Which thou hast exercised of old!
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
Remember not the faults and transgressions of my youth! According to thy mercy remember thou me, For thy goodness' sake, O LORD!
8 Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
Good and righteous is the LORD; Therefore showeth he to sinners the way.
9 Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
The humble he guideth in his statutes, And the humble he teacheth his way.
10 Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
All the doings of the LORD are mercy and truth To those who keep his covenant and his precepts.
11 Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
For thy name's sake, O LORD, Pardon my iniquity; for it is great!
12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
Who is the man that feareth the LORD? Him doth he show the way which he should choose.
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
He shall himself dwell in prosperity, And his offspring shall inherit the land.
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
The friendship of the LORD is with them that fear him, And he will teach them his covenant.
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
Mine eyes are ever directed to the LORD, For he will pluck my feet from the net.
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
Look upon me, and pity me; For I am desolate and afflicted!
17 Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
Lighten the sorrows of my heart, And deliver me from my troubles!
18 Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
Look upon my affliction and distress, And forgive all my sins!
19 Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
Consider how many are my enemies, And with what violence they hate me!
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
Guard thou my life, and deliver me! Let me not be put to shame, for I have trusted in thee!
21 Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
Let integrity and uprightness preserve me, For on thee do I rest my hope!
22 Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!
Redeem Israel, O God! from all his troubles!

< Zaburi 25 >