< Zaburi 25 >
1 Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
BY DAVID. [ALEPH-BET] To You, O YHWH, I lift up my soul.
2 Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
My God, in You I have trusted, Do not let me be ashamed, Do not let my enemies exult over me.
3 Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
Also let none waiting on You be ashamed, Let the treacherous dealers without cause be ashamed.
4 Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
Your ways, O YHWH, cause me to know, You teach me Your paths.
5 Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
Cause me to tread in Your truth, and teach me, For You [are] the God of my salvation, Near You I have waited all the day.
6 Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
Remember Your mercies, O YHWH, And Your kindnesses, for they [are] from the age.
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
Sins of my youth, and my transgressions, Do not remember. According to Your kindness be mindful of me, For Your goodness’ sake, O YHWH.
8 Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
Good and upright [is] YHWH, Therefore He directs sinners in the way.
9 Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
He causes the humble to tread in judgment, And teaches the humble His way.
10 Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
All the paths of YHWH [are] kindness and truth, To those keeping His covenant, And His testimonies.
11 Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
For Your Name’s sake, O YHWH, You have pardoned my iniquity, for it [is] great.
12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
Who [is] this—the man fearing YHWH? He directs him in the way He chooses.
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
His soul remains in good, And his seed possesses the land.
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
The secret of YHWH [is] for those fearing Him, And His covenant—to cause them to know.
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
My eyes [are] continually to YHWH, For He brings my feet out from a net.
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
Turn to me, and favor me, For I [am] lonely and afflicted.
17 Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
The distresses of my heart have enlarged themselves, Bring me out from my distresses.
18 Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
See my affliction and my misery, And bear with all my sins.
19 Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
See my enemies, for they have been many, And they have hated me with violent hatred.
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
Keep my soul, and deliver me, Do not let me be ashamed, for I trusted in You.
21 Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
Integrity and uprightness keep me, For I have waited [on] You.
22 Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!
Redeem Israel, O God, from all his distresses!