< Zaburi 25 >

1 Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
A Psalm of David. To you, O Lord, have I lifted up my soul.
2 Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
O my God, I have trusted in you: let me not be confounded, neither let mine enemies laugh me to scorn.
3 Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
For none of them that wait on you shall in any wise be ashamed: let them be ashamed that transgress without cause.
4 Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
Show me your ways, O Lord; and teach me your paths.
5 Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
Lead me in your truth, and teach me: for you are God my Saviour: and I have waited on you all the day.
6 Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
Remember your compassions, O Lord, and your mercies, for they are from everlasting.
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
Remember not the sins of my youth, nor [my sins] of ignorance: remember me according to your mercy, for your goodness' sake, O Lord.
8 Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
Good and upright is the Lord: therefore will he instruct sinners in [the] way.
9 Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
The meek will he guide in judgment: the meek will he teach his ways.
10 Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
All the ways of the Lord are mercy and truth to them that seek his covenant and his testimonies.
11 Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
For your name's sake, O Lord, do you also be merciful to my sin; for it is great.
12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
Who is the man that fears the Lord? he shall instruct him in the way which he has chosen.
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
His soul shall dwell in prosperity; and his seed shall inherit the earth.
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
The Lord is the strength of them that fear him; and his covenant is to manifest [truth] to them.
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
Mine eyes are continually to the Lord; for he shall draw my feet out of the snare.
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
Look upon me, and have mercy upon me; for I am an only child and poor.
17 Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
The afflictions of my heart have been multiplied; deliver me from my distresses.
18 Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
Look upon mine affliction and my trouble; and forgive all my sins.
19 Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
Look upon mine enemies; for they have been multiplied; and they have hated me with unjust hatred.
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
Keep my soul, and deliver me: let me not be ashamed; for I have hoped in you.
21 Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
The harmless and upright joined themselves to me: for I waited for you, O Lord.
22 Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!
Deliver Israel, O God, out of all his afflictions.

< Zaburi 25 >