< Zaburi 25 >
1 Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
Unto you, O LORD, do I lift up my soul.
2 Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
O my God, I trust in you: let me not be ashamed, let not mine enemies triumph over me.
3 Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
Yea, let none that wait on you be ashamed: let them be ashamed which transgress without cause.
4 Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
Show me your ways, O LORD; teach me your paths.
5 Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
Lead me in your truth, and teach me: for you are the God of my salvation; on you do I wait all the day.
6 Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
Remember, O LORD, your tender mercies and your loving kindnesses; for they have been ever of old.
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
Remember not the sins of my youth, nor my transgressions: according to your mercy remember you me for your goodness' sake, O LORD.
8 Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
Good and upright is the LORD: therefore will he teach sinners in the way.
9 Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
The meek will he guide in judgment: and the meek will he teach his way.
10 Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
All the paths of the LORD are mercy and truth unto such as keep his covenant and his testimonies.
11 Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
For your name's sake, O LORD, pardon mine iniquity; for it is great.
12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
What man is he that fears the LORD? him shall he teach in the way that he shall choose.
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
His soul shall dwell at ease; and his seed shall inherit the earth.
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
The secret of the LORD is with them that fear him; and he will show them his covenant.
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
Mine eyes are ever toward the LORD; for he shall pluck my feet out of the net.
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
Turn you unto me, and have mercy upon me; for I am desolate and afflicted.
17 Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
The troubles of my heart are enlarged: O bring you me out of my distresses.
18 Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
Look upon mine affliction and my pain; and forgive all my sins.
19 Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
Consider mine enemies; for they are many; and they hate me with cruel hatred.
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
O keep my soul, and deliver me: let me not be ashamed; for I put my trust in you.
21 Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
Let integrity and uprightness preserve me; for I wait on you.
22 Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!
Redeem Israel, O God, out of all his troubles.