< Zaburi 24 >

1 Nchi ni ya Yahwe, na vyote viijazavyo, dunia, na wote wakaao ndani yake.
مزمور داود زمین و پری آن از آن خداوند است. ربع مسکون و ساکنان آن.۱
2 Kwa kuwa yeye aliianzisha juu ya bahari na kuiimarisha juu ya mito.
زیرا که اواساس آن را بر دریاها نهاد. و آن را بر نهرها ثابت گردانید.۲
3 Ni nani atakaye panda mlima wa Yahwe? Ni nani atakaye simama patakatifu pake?
کیست که به کوه خداوند برآید؟ وکیست که به مکان قدس او ساکن شود؟۳
4 Yeye ambaye ana mikono misafi na moyo safi; ambaye hajauinua uongo, na haja apa kiapo ili kudanganya.
او که پاک دست و صاف دل باشد، که جان خود را به بطالت ندهد و قسم دروغ نخورد.۴
5 Yeye atapokea baraka kutoka kwa Yahwe na haki kutoka kwa Mungu wa wokovu wake.
او برکت را ازخداوند خواهد یافت. و عدالت را از خدای نجات خود.۵
6 Kizazi cha wale wamtafutao Mungu ni kama hiki, wale ambao wanautafuta uso wa Mungu wa Yakobo.
این است طبقه طالبان او. طالبان روی تو‌ای (خدای ) یعقوب. سلاه.۶
7 Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
‌ای دروازه‌ها سرهای خود را برافرازید! ای درهای ابدی برافراشته شوید تا پادشاه جلال داخل شود!۷
8 Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe, mwenye nguvu na uweza; Yahwe, mwenye uweza katika vita.
این پادشاه جلال کیست؟ خداوندقدیر و جبار؟ خداوند که در جنگ جبار است.۸
9 Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
‌ای دروازه‌ها، سرهای خود را برافرازید! ای درهای ابدی برافرازید تا پادشاه جلال داخل شود!۹
10 Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe wa majeshi, yeye ni Mfalme wa utukufu.
این پادشاه جلال کیست؟ یهوه صبایوت پادشاه جلال اوست. سلاه.۱۰

< Zaburi 24 >