< Zaburi 24 >
1 Nchi ni ya Yahwe, na vyote viijazavyo, dunia, na wote wakaao ndani yake.
“A psalm of David.” The earth is the LORD'S, and all that is therein; The world, and they who inhabit it.
2 Kwa kuwa yeye aliianzisha juu ya bahari na kuiimarisha juu ya mito.
For he hath founded it upon the seas, And established it upon the floods.
3 Ni nani atakaye panda mlima wa Yahwe? Ni nani atakaye simama patakatifu pake?
Who shall ascend the hill of the LORD? And who shall stand in his holy place?
4 Yeye ambaye ana mikono misafi na moyo safi; ambaye hajauinua uongo, na haja apa kiapo ili kudanganya.
He that hath clean hands and a pure heart; Who hath not inclined his soul to falsehood, Nor sworn deceitfully.
5 Yeye atapokea baraka kutoka kwa Yahwe na haki kutoka kwa Mungu wa wokovu wake.
He shall receive a blessing from the LORD, And favor from the God of his salvation.
6 Kizazi cha wale wamtafutao Mungu ni kama hiki, wale ambao wanautafuta uso wa Mungu wa Yakobo.
This is the race of them that seek him; They that seek thy face are Jacob. (Pause)
7 Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
Lift up your heads, O ye gates! Lift yourselves up, ye everlasting doors, That the king of glory may come in!
8 Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe, mwenye nguvu na uweza; Yahwe, mwenye uweza katika vita.
“Who is this king of glory?” Jehovah, strong and mighty; Jehovah, mighty in battle.
9 Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
Lift up your heads, O ye gates! Lift yourselves up, ye everlasting doors, That the king of glory may enter in!
10 Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe wa majeshi, yeye ni Mfalme wa utukufu.
“Who is this king of glory?” Jehovah, God of hosts, he is the king of glory. (Pause)