< Zaburi 23 >
1 Yahwe ni mchungaji wangu; sita pungukiwa na kitu.
“A psalm of David.” The LORD is my shepherd: I shall not want.
2 Yeye hunilaza katika majani mabichi; huniongoza kando ya maji matulivu.
He maketh me to lie down in green pastures; He leadeth me beside the still waters.
3 Yeye huurejesha uhai wangu; huniongoza katika njia iliyo sahihi kwa ajili ya jina lake.
He reviveth my soul; He leadeth me in paths of safety, For his name's sake.
4 Hata ijapokuwa nikipita katika bonde la uvuli na giza nene, sitaogopa kudhurika kwa kuwa wewe uko pamoja nami; fimbo yako na gongo lako vya nifariji.
When I walk through a valley of deathlike shade, I fear no evil; for thou art with me; Thy crook and thy staff, they comfort me.
5 Wewe waandaa meza mbele yangu katika uwepo wa maadui zangu; umenipaka mafuta kichwa changu na kikombe changu kinafurika.
Thou preparest a table before me In the presence of mine enemies. Thou anointest my head with oil; My cup runneth over.
6 Hakika wema na uaminifu wa agano vitaniandama siku zote za maisha yangu; nami nitaishi katika nyumba ya Yahwe milele!
Surely goodness and mercy shall follow me all the days of my life, And I shall dwell in the house of the LORD for ever.