< Zaburi 22 >

1 Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
Au chef des chantres. D’Après l’Ayyélet Hachahar. Psaume de David. Mon Dieu, mon Dieu, pourquoi m’as-tu abandonné, loin de me porter secours, d’entendre mes paroles suppliantes?
2 Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
Mon Dieu, j’appelle de jour et tu ne réponds pas, de nuit, et il n’est pas de trêve pour moi.
3 Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
Tu es pourtant le Saint, trônant au milieu des louanges d’Israël.
4 Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
En toi nos pères ont eu confiance, ils ont eu confiance, et tu les as sauvés.
5 Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
Ils ont crié vers toi et ont été délivrés; ils ont espéré en toi et n’ont pas été déçus.
6 Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
Moi, je suis un vermisseau, et non un homme, l’opprobre des gens, objet de mépris pour le peuple.
7 Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
Tous ceux qui me voient se moquent de moi, grimacent des lèvres, hochent la tête.
8 Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
"Qu’il s’en remette à l’Eternel! Que celui-ci le sauve, qu’il l’arrache du danger, puisqu’il l’aime!"
9 Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
Oui, c’est toi qui m’as tiré des entrailles maternelles, qui m’as fait reposer en sûreté dans le giron de ma mère;
10 Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
entre tes bras j’ai été jeté dès ma naissance, dès le sein de ma mère, tu as été mon Dieu.
11 Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
Ne t’éloigne pas de moi car l’angoisse est proche, et nul n’est là pour m’aider.
12 Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
Des taureaux nombreux m’environnent, des bêtes puissantes de Basan m’assiègent.
13 Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
Ils ouvrent contre moi leur gueule, tel un lion qui déchire et qui rugit.
14 Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
Je suis comme l’eau qu’on répand, tous mes membres se disloquent; mon cœur est comme de la cire, qui fondrait au milieu de mes entrailles.
15 Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
Ma sève est desséchée comme un tesson, ma langue est collée à mon palais; tu m’étends dans la poussière de la mort.
16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
Car des chiens m’enveloppent, la bande des méchants fait cercle autour de moi; comme le lion ils meurtrissent mes mains et mes pieds.
17 Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
Je pourrais compter tous mes os; eux, ils me toisent et se repaissent de ma vue.
18 Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
Ils se partagent mes habits, ils tirent au sort mes vêtements.
19 Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
Mais toi, ô Seigneur, ne t’éloigne pas; toi, qui es ma force, viens vite à mon secours!
20 Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
Sauve mon âme du glaive, ma vie de la fureur des chiens;
21 Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
arrache-moi de la gueule du lion, protège-moi contre les cornes des buffles.
22 Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
Je proclamerai ton nom devant mes frères, au milieu de l’assemblée, je te louerai.
23 Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
"Adorateurs de l’Eternel, louez-le vous tous, descendants de Jacob, honorez-le; révérez-le, vous tous, postérité d’Israël!
24 Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
Car il n’a point dédaigné, il n’a point méprisé la misère du malheureux; il n’a pas caché de lui son visage, ni manqué de l’entendre quand il implorait!"
25 Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
C’Est toi dont je célébrerai les louanges dans la grande assemblée, j’accomplirai mes vœux devant ceux qui te craignent.
26 Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
Les humbles mangeront et seront rassasiés, les adorateurs de l’Eternel le loueront. Que votre cœur renaisse à la vie pour toujours!
27 Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
Les confins de la terre se souviendront et reviendront au Seigneur, toutes les familles des peuples se prosterneront devant lui.
28 Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
Car à l’Eternel appartient la royauté, il domine sur toutes les nations.
29 Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
Ils mangeront et adoreront, tous les heureux de la terre; devant lui s’inclineront ceux qui descendent dans la poussière, incapables de sustenter leur vie.
30 Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
La postérité lui vouera un culte; on parlera du Seigneur aux âges à venir.
31 Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!
IIs viendront et proclameront sa justice: ils diront au peuple à naître ce qu’il a fait.

< Zaburi 22 >