< Zaburi 22 >

1 Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
My God, my God, why have you abandoned/deserted me? Why do you stay so far from me, and why do you not hear/help me [RHQ]? Why do you not hear me when I am groaning?
2 Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
My God, every day I call to you during the daytime and during the night, but you do not answer me, so I am not able to sleep.
3 Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
But you are holy. You sit on your throne as king, and [we the people of] Israel praise you [PRS].
4 Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
Our ancestors trusted in you. [Because] they trusted in you, you rescued them.
5 Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
When they cried out to you, you saved them. They trusted in you, and (they were not disappointed/you [saved them] as you said that you would).
6 Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
But [you have not rescued me] [People despise me and consider that I am not a man]; [they think that] I am [as worthless as] a worm! Everyone [HYP] scorns me and despises me.
7 Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
Everyone who sees me [HYP] makes fun of me. They sneer at me and [insult me by] shaking their heads [at me as though I were an evil man]. They say,
8 Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
“He trusts in Yahweh, so Yahweh should save him! [He says that] Yahweh is very pleased with him; if that is so, Yahweh should rescue him!”
9 Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
[Why do] you [not] protect me [now as you did] when I was born? I was safe even when I was (nursing/drinking milk from my mother’s breasts).
10 Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
[It was as though] you adopted me right when I was born. You have (been my God/taken care of me) ever since I was born.
11 Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
So, (do not stay far from/stay close to) [LIT] me now because [enemies who will cause me much] trouble are near me, and there is no one [else] who can help me.
12 Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
[My enemies] surround me [like] a herd/group of wild bulls. [Fierce people, like those] strong bulls that graze [on the hills] in Bashan [area], encircle me.
13 Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
[They are like] roaring lions that are attacking the animals that they want to kill [MET] [and eat]; they rush toward me [to kill] me; they [are like lions that] have their mouths open, [ready to tear their victims to pieces] [MET].
14 Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
I am completely exhausted [MET], and all my bones are out of their joints/places. I [no longer expect that God will save me]; [that expectation is gone completely], like wax that has melted away.
15 Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
My strength is [all dried up] [MET] like a broken piece of a clay jar that has dried [in the sun]. [I am so thirsty that] my tongue sticks to the roof of my mouth. O God, [I think that you are about to let] me die and become dirt!
16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
My enemies [MET] surround me like a pack/group of wild dogs. A group of evil men has encircled me, [ready to attack me]. They have [already] smashed my hands and my feet.
17 Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
[I am so weak and thin that] my bones can be seen and counted. My enemies stare at me and (gloat/are happy) about [what has happened to] me.
18 Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
They looked at the clothes that I [was wearing] and gambled to determine which piece each of them would get.
19 Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
O Yahweh, do not stay far away from me! You who are my [source of] strength, come quickly and help me!
20 Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
Rescue me from [those who want to kill me with] their swords. Save me from those who are [like wild/fierce] dogs [MET].
21 Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
Snatch me away from [my enemies who are] like lions whose jaws [are already open, ready to chew me up] Grab me away from [those men who are like] wild oxen [that attack other animals with] their horns [MET]!
22 Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
[But you have saved me, so] I will declare to my fellow [Israelis] how great you [MTY] are. I will praise you among the group of your people gathered [to worship you].
23 Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
You people who have an awesome respect for Yahweh, praise him! All you who are descended from Jacob, honor Yahweh! All you Israeli people, revere him!
24 Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
He does not despise or ignore those who are suffering; he does not hide (his face/himself) from them. He has listened to them when they cried out to him for help.
25 Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
Yahweh, in the great gathering [of your people], I will praise you for what you have done. In the presence of those who revere you, I will offer [the sacrifices] that I promised.
26 Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
The poor people [whom I have invited to the meal] will eat as much as they want. All who come worship Yahweh will praise him. I pray that [God will enable] you all to live a long and happy life!
27 Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
I pray that [people in all nations, even] in the remote areas, will think about Yahweh and turn to him, and that people from all the clans in the world will bow down before him.
28 Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
Because Yahweh is the king! He rules all the nations.
29 Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
I desire that all the rich people on the earth will bow before him. Some day they will die, but I want them to prostrate themselves on the ground in his presence [before they die].
30 Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
People (in the future generations/who have not been born yet) will also serve Yahweh. Our descendants will be told about what Yahweh [has done].
31 Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!
People who are not yet born, [who will live in future years], will be told how Yahweh rescued his people. People will tell them, “Yahweh did it!”

< Zaburi 22 >