< Zaburi 22 >

1 Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
To the Chief Musician. On "the Hind of the Dawn." A Melody of David. My GOD, my GOD, why hast thou forsaken me? Far from saving me, The words of my loud lamentation?
2 Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
My God! I keep crying—By day, and thou dost not answer, and, By night, and there is no rest for me.
3 Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
But, thou, art holy, Who inhabitest the praises of Israel.
4 Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
In thee, trusted our fathers, They trusted, and thou didst deliver them;
5 Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
Unto thee, made they outcry, and escaped, In thee, they trusted, and had not turned pale.
6 Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
But, I, am a worm and no one, a reproach of men, and despised of a people;
7 Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
All that see me, laugh at me, —They open wide the mouth, They shake the head: —
8 Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
He should trust in Yahweh—let him deliver him, —Let him rescue him, seeing he delighteth in him.
9 Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
For, thou, art he that severed me from the womb, he that caused me to trust, upon the breasts of my mother;
10 Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
Upon thee, was I cast from the time I was born, From the womb of my mother, my GOD, hast thou been.
11 Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
Be not far from me, for, distress, is near, For there is none to help.
12 Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
Many bulls have surrounded me, Strong oxen of Bashan, have enclosed me;
13 Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
They have opened wide against me their mouth, A lion rending and roaring.
14 Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
Like water, am I poured out, and, put out of joint, are all my bones, —My heart, hath become, like wax, it is melted in the midst of my body;
15 Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
Dried as a potsherd, is my strength, And, my tongue, is made to cleave to my gums, And, in the dust of death, wilt thou lay me.
16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
For dogs have surrounded me, —An assembly of evil doers, have encircled me, They have pierced my hands and my feet,
17 Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
I may tell all my bones, They, look for—they behold me!
18 Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
They part my garments among them, and, for my vestment, they cast lots.
19 Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
But, thou, O Yahweh, be not far off, O my help! to aid me, make haste;
20 Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
Rescue, from the sword, my life, from the power of the dog, my solitary self:
21 Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
Save me from the mouth of the lion, —Yea, from the horns of wild beasts, hast thou delivered me.
22 Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
I will declare thy Name unto my brethren, —In the midst of the convocation, will I praise thee.
23 Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
Ye that revere Yahweh, praise him, All ye the seed of Jacob, glorify him, And, stand in awe of him, all ye seed of Israel.
24 Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
For he hath not despised nor abhorred the humbling of the patient one, neither hath he hid his face from him, but, when he cried for help unto him, he heard.
25 Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
Of thee, is my praise in the great convocation, My vows, will I pay, before them who revere him.
26 Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
The patient wronged-ones shall eat and be satisfied, They shall praise Yahweh, who are seekers of him, Let your heart live for aye.
27 Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
All the ends of the earth, will remember and turn to Yahweh, Yea all the families of the nations, will bow themselves down before thee,
28 Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
For, to Yahweh, belongeth the kingdom, And One to Rule over the nations.
29 Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
All the great ones of the earth, shall eat and bow down, Before him shall kneel, all that go down to the dust, Even he who had not kept alive, his own soul!
30 Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
My seed, shall serve him, It shall be recounted, of the Lord, to a generation that shall come:
31 Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!
That his righteousness may be declared to a people to be born, That he wrought with effect!

< Zaburi 22 >