< Zaburi 22 >

1 Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
My God, my God, why have you forsaken me? why are you so far from helping me, and from the words of my roaring?
2 Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
O my God, I cry in the day time, but you hear not; and in the night season, and am not silent.
3 Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
But you are holy, O you that inhabit the praises of Israel.
4 Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
Our fathers trusted in you: they trusted, and you did deliver them.
5 Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
They cried to you, and were delivered: they trusted in you, and were not confounded.
6 Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
But I am a worm, and no man; a reproach of men, and despised of the people.
7 Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
All they that see me laugh me to scorn: they shoot out the lip, they shake the head, saying,
8 Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
He trusted on the LORD that he would deliver him: let him deliver him, seeing he delighted in him.
9 Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
But you are he that took me out of the womb: you did make me hope when I was on my mother’s breasts.
10 Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
I was cast on you from the womb: you are my God from my mother’s belly.
11 Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
Be not far from me; for trouble is near; for there is none to help.
12 Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
Many bulls have compassed me: strong bulls of Bashan have beset me round.
13 Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
They gaped on me with their mouths, as a ravening and a roaring lion.
14 Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
I am poured out like water, and all my bones are out of joint: my heart is like wax; it is melted in the middle of my bowels.
15 Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
My strength is dried up like a potsherd; and my tongue sticks to my jaws; and you have brought me into the dust of death.
16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
For dogs have compassed me: the assembly of the wicked have enclosed me: they pierced my hands and my feet.
17 Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
I may tell all my bones: they look and stare on me.
18 Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
They part my garments among them, and cast lots on my clothing.
19 Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
But be not you far from me, O LORD: O my strength, haste you to help me.
20 Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
Deliver my soul from the sword; my darling from the power of the dog.
21 Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
Save me from the lion’s mouth: for you have heard me from the horns of the unicorns.
22 Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
I will declare your name to my brothers: in the middle of the congregation will I praise you.
23 Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
You that fear the LORD, praise him; all you the seed of Jacob, glorify him; and fear him, all you the seed of Israel.
24 Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
For he has not despised nor abhorred the affliction of the afflicted; neither has he hid his face from him; but when he cried to him, he heard.
25 Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
My praise shall be of you in the great congregation: I will pay my vows before them that fear him.
26 Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
The meek shall eat and be satisfied: they shall praise the LORD that seek him: your heart shall live for ever.
27 Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
All the ends of the world shall remember and turn to the LORD: and all the kindreds of the nations shall worship before you.
28 Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
For the kingdom is the LORD’s: and he is the governor among the nations.
29 Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
All they that be fat on earth shall eat and worship: all they that go down to the dust shall bow before him: and none can keep alive his own soul.
30 Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
A seed shall serve him; it shall be accounted to the Lord for a generation.
31 Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!
They shall come, and shall declare his righteousness to a people that shall be born, that he has done this.

< Zaburi 22 >