< Zaburi 22 >

1 Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
Unto the end, for the morning protection, a psalm for David. O God my God, look upon me: why hast thou forsaken me? Far from my salvation are the words of my sins.
2 Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
O my God, I shall cry by day, and thou wilt not hear: and by night, and it shall not be reputed as folly in me.
3 Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
But thou dwellest in the holy place, the praise of Israel.
4 Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
In thee have our fathers hoped: they have hoped, and thou hast delivered them.
5 Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
They cried to thee, and they were saved: they trusted in thee, and were not confounded.
6 Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
But I am a worm, and no man: the reproach of men, and the outcast of the people.
7 Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
All they that saw me have laughed me to scorn: they have spoken with the lips, and wagged the head.
8 Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
He hoped in the Lord, let him deliver him: let him save him, seeing he delighteth in him.
9 Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
For thou art he that hast drawn me out of the womb: my hope from the breasts of my mother.
10 Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
I was cast upon thee from the womb. From my mother’s womb thou art my God,
11 Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
Depart not from me. For tribulation is very near: for there is none to help me.
12 Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
Many calves have surrounded me: fat bulls have besieged me.
13 Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
They have opened their mouths against me, as a lion ravening and roaring.
14 Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
I am poured out like water; and all my bones are scattered. My heart is become like wax melting in the midst of my bowels.
15 Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
My strength is dried up like a potsherd, and my tongue hath cleaved to my jaws: and thou hast brought me down into the dust of death.
16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
For many dogs have encompassed me: the council of the malignant hath besieged me. They have dug my hands and feet.
17 Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
They have numbered all my bones. And they have looked and stared upon me.
18 Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
They parted my garments amongst them; and upon my vesture they cast lots.
19 Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
But thou, O Lord, remove not thy help to a distance from me; look towards my defence.
20 Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
Deliver, O God, my soul from the sword: my only one from the hand of the dog.
21 Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
Save me from the lion’s mouth; and my lowness from the horns of the unicorns.
22 Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
I will declare thy name to my brethren: in the midst of the church will I praise thee.
23 Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
Ye that fear the Lord, praise him: all ye the seed of Jacob, glorify him.
24 Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
Let all the seed of Israel fear him: because he hath not slighted nor despised the supplication of the poor man. Neither hath he turned away his face from me: and when I cried to him he heard me.
25 Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
With thee is my praise in a great church: I will pay my vows in the sight of them that fear him.
26 Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
The poor shall eat and shall be filled: and they shall praise the Lord that seek him: their hearts shall live for ever and ever.
27 Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
All the ends of the earth shall remember, and shall be converted to the Lord: And all the kindreds of the Gentiles shall adore in his sight.
28 Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
For the kingdom is the Lord’s; and he shall have dominion over the nations.
29 Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
All the fat ones of the earth have eaten and have adored: all they that go down to the earth shall fall before him.
30 Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
And to him my soul shall live: and my seed shall serve him.
31 Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!
There shall be declared to the Lord a generation to come: and the heavens shall shew forth his justice to a people that shall be born, which the Lord hath made.

< Zaburi 22 >