< Zaburi 22 >

1 Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
大卫的诗,交与伶长。调用朝鹿。 我的 神,我的 神!为什么离弃我? 为什么远离不救我?不听我唉哼的言语?
2 Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
我的 神啊,我白日呼求,你不应允, 夜间呼求,并不住声。
3 Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
但你是圣洁的, 是用以色列的赞美为宝座的。
4 Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
我们的祖宗倚靠你; 他们倚靠你,你便解救他们。
5 Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
他们哀求你,便蒙解救; 他们倚靠你,就不羞愧。
6 Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
但我是虫,不是人, 被众人羞辱,被百姓藐视。
7 Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
凡看见我的都嗤笑我; 他们撇嘴摇头,说:
8 Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
他把自己交托耶和华,耶和华可以救他吧! 耶和华既喜悦他,可以搭救他吧!
9 Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
但你是叫我出母腹的; 我在母怀里,你就使我有倚靠的心。
10 Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
我自出母胎就被交在你手里; 从我母亲生我,你就是我的 神。
11 Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
求你不要远离我! 因为急难临近了,没有人帮助我。
12 Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
有许多公牛围绕我, 巴珊大力的公牛四面困住我。
13 Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
它们向我张口, 好像抓撕吼叫的狮子。
14 Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
我如水被倒出来; 我的骨头都脱了节; 我心在我里面如蜡熔化。
15 Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
我的精力枯干,如同瓦片; 我的舌头贴在我牙床上。 你将我安置在死地的尘土中。
16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
犬类围着我,恶党环绕我; 他们扎了我的手,我的脚。
17 Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
我的骨头,我都能数过; 他们瞪着眼看我。
18 Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
他们分我的外衣, 为我的里衣拈阄。
19 Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
耶和华啊,求你不要远离我! 我的救主啊,求你快来帮助我!
20 Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
求你救我的灵魂脱离刀剑, 救我的生命脱离犬类,
21 Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
救我脱离狮子的口; 你已经应允我,使我脱离野牛的角。
22 Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
我要将你的名传与我的弟兄, 在会中我要赞美你。
23 Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
你们敬畏耶和华的人要赞美他! 雅各的后裔都要荣耀他! 以色列的后裔都要惧怕他!
24 Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
因为他没有藐视憎恶受苦的人, 也没有向他掩面; 那受苦之人呼吁的时候,他就垂听。
25 Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
我在大会中赞美你的话是从你而来的; 我要在敬畏耶和华的人面前还我的愿。
26 Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
谦卑的人必吃得饱足; 寻求耶和华的人必赞美他。 愿你们的心永远活着!
27 Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
地的四极都要想念耶和华,并且归顺他; 列国的万族都要在你面前敬拜。
28 Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
因为国权是耶和华的; 他是管理万国的。
29 Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
地上一切丰肥的人必吃喝而敬拜; 凡下到尘土中—不能存活自己性命的人 —都要在他面前下拜。
30 Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
他必有后裔事奉他; 主所行的事必传与后代。
31 Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!
他们必来把他的公义传给将要生的民, 言明这事是他所行的。

< Zaburi 22 >