< Zaburi 21 >

1 Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. Mfalme anashangilia katika uweza wako, Yahwe! Ni kwa namna kuu anashangilia katika wokovu uliouleta!
Oh Yavé, el rey se alegrará en tu poder, Y en tu salvación ¡cuánto se regocijará!
2 Wewe umempa yeye matamanio ya moyo wake na hauja mkatalia maombi midomo yake.
Le diste el deseo de su corazón Y no le retuviste la petición de sus labios. (Selah)
3 Kwa kuwa wewe unamletea baraka nyingi; wewe uliweka katika kichwa chake taji ya dhahabu iliyo safi kabisa.
Con bendiciones de bien saliste a su encuentro. Corona de oro puro pusiste en su cabeza.
4 Yeye alikuomba wewe maisha; ukampatia maisha; wewe ulimpatia maisha malefu milele na milele.
Vida te pidió, Y se la concediste, Largura de días, eternamente y para siempre.
5 Yeye utukufu wake ni mkuu kwa sababu ya ushindi wako; wewe umemuwekea mapambo na enzi.
Grande es su gloria por tu salvación. Pusiste sobre él honor y majestad.
6 Kwa kuwa unampatia yeye baraka za kudumu; unamfurahisha kwa furaha ya uwepo wako.
Lo bendijiste para siempre. Lo llenaste de alegría con tu Presencia
7 Kwa kuwa Mfalme humwamini Yahwe; kwa kupitia uaminifu wa agano la aliye juu zaidi yeye hataondolewa.
Por cuanto el rey confía en Yavé. Por la misericordia de ʼElyón, no será conmovido.
8 Mkono wako utawakamata adui zangu wote wote; mkono wako wa kuume utawakamata wale wote wanao kuchukia.
Tu mano alcanzará a todos tus enemigos. Tu mano derecha alcanzará a los que te aborrecen.
9 Wakati wa hasira yako, wewe utawachoma kama katika tanuru la moto. Yahwe atawamaliza wao katika hasira yake, na moto utawateketeza upesi wao.
Los pondrás en horno de fuego en el tiempo de tu ira. Yavé los deshará en su ira, Y el fuego los consumirá.
10 Wewe utawaangamiza watoto wao duniani na ukoo wao kutoka katika mrorongo wa wanadamu.
Destruirás su producto de la tierra, Y su descendencia de entre los hijos de hombres.
11 Kwa kuwa walikusudia kukufanyia mambo maovu wewe; wao walitunga njama ambayo kwayo hawawezi kufanikiwa!
Porque tramaron el mal contra Ti. Fraguaron un complot, Pero no prevalecerán.
12 Kwa kuwa wewe utawarudisha nyuma; wewe utafyatua upinde wako mbele yao.
Pues Tú les harás volver la espalda Al apuntar tu arco contra sus rostros.
13 Uninuliwe, Yahwe, katika uweza wako; tutaimba na kusifu nguvu zako.
¡Engrandécete, oh Yavé, con tu fortaleza! Cantaremos y alabaremos tu poderío.

< Zaburi 21 >