< Zaburi 21 >

1 Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. Mfalme anashangilia katika uweza wako, Yahwe! Ni kwa namna kuu anashangilia katika wokovu uliouleta!
למנצח מזמור לדוד יהוה בעזך ישמח מלך ובישועתך מה יגיל מאד׃
2 Wewe umempa yeye matamanio ya moyo wake na hauja mkatalia maombi midomo yake.
תאות לבו נתתה לו וארשת שפתיו בל מנעת סלה׃
3 Kwa kuwa wewe unamletea baraka nyingi; wewe uliweka katika kichwa chake taji ya dhahabu iliyo safi kabisa.
כי תקדמנו ברכות טוב תשית לראשו עטרת פז׃
4 Yeye alikuomba wewe maisha; ukampatia maisha; wewe ulimpatia maisha malefu milele na milele.
חיים שאל ממך נתתה לו ארך ימים עולם ועד׃
5 Yeye utukufu wake ni mkuu kwa sababu ya ushindi wako; wewe umemuwekea mapambo na enzi.
גדול כבודו בישועתך הוד והדר תשוה עליו׃
6 Kwa kuwa unampatia yeye baraka za kudumu; unamfurahisha kwa furaha ya uwepo wako.
כי תשיתהו ברכות לעד תחדהו בשמחה את פניך׃
7 Kwa kuwa Mfalme humwamini Yahwe; kwa kupitia uaminifu wa agano la aliye juu zaidi yeye hataondolewa.
כי המלך בטח ביהוה ובחסד עליון בל ימוט׃
8 Mkono wako utawakamata adui zangu wote wote; mkono wako wa kuume utawakamata wale wote wanao kuchukia.
תמצא ידך לכל איביך ימינך תמצא שנאיך׃
9 Wakati wa hasira yako, wewe utawachoma kama katika tanuru la moto. Yahwe atawamaliza wao katika hasira yake, na moto utawateketeza upesi wao.
תשיתמו כתנור אש לעת פניך יהוה באפו יבלעם ותאכלם אש׃
10 Wewe utawaangamiza watoto wao duniani na ukoo wao kutoka katika mrorongo wa wanadamu.
פרימו מארץ תאבד וזרעם מבני אדם׃
11 Kwa kuwa walikusudia kukufanyia mambo maovu wewe; wao walitunga njama ambayo kwayo hawawezi kufanikiwa!
כי נטו עליך רעה חשבו מזמה בל יוכלו׃
12 Kwa kuwa wewe utawarudisha nyuma; wewe utafyatua upinde wako mbele yao.
כי תשיתמו שכם במיתריך תכונן על פניהם׃
13 Uninuliwe, Yahwe, katika uweza wako; tutaimba na kusifu nguvu zako.
רומה יהוה בעזך נשירה ונזמרה גבורתך׃

< Zaburi 21 >