< Zaburi 20 >
1 Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. Mungu akusaidie wakati wa shida; na jina la Mungu wa Yakobo likulinde
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Bwana na akujibu unapokuwa katika dhiki, jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako.
2 na kutuma msaada kutoka mahali patakatifu kwa ajili ya kukutegemeza wewe kutoka Sayuni.
Na akutumie msaada kutoka patakatifu na akupatie msaada kutoka Sayuni.
3 Naye akumbuke sadaka yako yote na kuipokea sadaka ya kuteketezwa.
Na azikumbuke dhabihu zako zote, na azikubali sadaka zako za kuteketezwa.
4 Naye akujalie haja za moyo wako na kutimiza mipango yako yote.
Na akujalie haja ya moyo wako, na aifanikishe mipango yako yote.
5 Ndipo tutakapo shangilia katika ushindi wako, na, katika jina la Mungu wetu, tutapeperusha bendera. Yahwe naakupe maombi yako yote ya haki.
Tutashangilia kwa furaha utakaposhinda, tutainua bendera zetu kwa jina la Mungu wetu. Bwana na akupe haja zako zote.
6 Sasa ninajua ya kuwa Yahwe atawaokoa wapakwa mafuta wake; yeye atamjibu yeye kutoka katika mbingu takatifu kwa uweza wa mkono wake wa kuume ambao waweza kumuokoa yeye.
Sasa nafahamu kuwa Bwana humwokoa mpakwa mafuta wake, humjibu kutoka mbingu yake takatifu kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume.
7 Baadhi hamini katika magari na wengine katika farasi, lakini sisi tumuita Yahwe Mungu wetu.
Wengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi, bali sisi tutalitumainia jina la Bwana, Mungu wetu.
8 Wao watashushwa chini na kuanguka, bali sisi tutainuka na kusimama wima!
Wao wameshushwa chini na kuanguka, bali sisi tunainuka na kusimama imara.
9 Yahwe, umuokoe mfalme; utusaidie sisi tukuitapo.
Ee Bwana, mwokoe mfalme! Tujibu tunapokuita!