< Zaburi 20 >

1 Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. Mungu akusaidie wakati wa shida; na jina la Mungu wa Yakobo likulinde
For the chief musician. A psalm of David. May Yahweh help you in the day of trouble; may the name of the God of Jacob protect you
2 na kutuma msaada kutoka mahali patakatifu kwa ajili ya kukutegemeza wewe kutoka Sayuni.
and send help from the holy place to support you from Zion.
3 Naye akumbuke sadaka yako yote na kuipokea sadaka ya kuteketezwa.
May he call to mind all your offerings and accept your burnt sacrifice. (Selah)
4 Naye akujalie haja za moyo wako na kutimiza mipango yako yote.
May he grant you your heart's desire and fulfill all your plans.
5 Ndipo tutakapo shangilia katika ushindi wako, na, katika jina la Mungu wetu, tutapeperusha bendera. Yahwe naakupe maombi yako yote ya haki.
Then we will rejoice in your victory, and, in the name of our God, we will raise banners. May Yahweh grant all your petitions.
6 Sasa ninajua ya kuwa Yahwe atawaokoa wapakwa mafuta wake; yeye atamjibu yeye kutoka katika mbingu takatifu kwa uweza wa mkono wake wa kuume ambao waweza kumuokoa yeye.
Now I know that Yahweh will rescue his anointed one; he will answer him from his holy heaven with the strength of his right hand that can rescue him.
7 Baadhi hamini katika magari na wengine katika farasi, lakini sisi tumuita Yahwe Mungu wetu.
Some trust in chariots and others in horses, but we call on Yahweh our God.
8 Wao watashushwa chini na kuanguka, bali sisi tutainuka na kusimama wima!
They will be brought down and fall, but we will rise and stand upright!
9 Yahwe, umuokoe mfalme; utusaidie sisi tukuitapo.
Yahweh, rescue the king; help us when we call.

< Zaburi 20 >