< Zaburi 20 >

1 Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. Mungu akusaidie wakati wa shida; na jina la Mungu wa Yakobo likulinde
For the choirmaster. A Psalm of David. May the LORD answer you in the day of trouble; may the name of the God of Jacob protect you.
2 na kutuma msaada kutoka mahali patakatifu kwa ajili ya kukutegemeza wewe kutoka Sayuni.
May He send you help from the sanctuary and sustain you from Zion.
3 Naye akumbuke sadaka yako yote na kuipokea sadaka ya kuteketezwa.
May He remember all your gifts and look favorably on your burnt offerings.
4 Naye akujalie haja za moyo wako na kutimiza mipango yako yote.
May He give you the desires of your heart and make all your plans succeed.
5 Ndipo tutakapo shangilia katika ushindi wako, na, katika jina la Mungu wetu, tutapeperusha bendera. Yahwe naakupe maombi yako yote ya haki.
May we shout for joy at your victory and raise a banner in the name of our God. May the LORD grant all your petitions.
6 Sasa ninajua ya kuwa Yahwe atawaokoa wapakwa mafuta wake; yeye atamjibu yeye kutoka katika mbingu takatifu kwa uweza wa mkono wake wa kuume ambao waweza kumuokoa yeye.
Now I know that the LORD saves His anointed; He answers him from His holy heaven with the saving power of His right hand.
7 Baadhi hamini katika magari na wengine katika farasi, lakini sisi tumuita Yahwe Mungu wetu.
Some trust in chariots and others in horses, but we trust in the name of the LORD our God.
8 Wao watashushwa chini na kuanguka, bali sisi tutainuka na kusimama wima!
They collapse and fall, but we rise up and stand firm.
9 Yahwe, umuokoe mfalme; utusaidie sisi tukuitapo.
O LORD, save the king. Answer us on the day we call.

< Zaburi 20 >