< Zaburi 2 >

1 Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
Was soll das Toben der Völker und das eitle Sinnen der Völkerschaften?
2 Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
Die Könige der Erde rotten sich zusammen, und die Fürsten halten Rat miteinander gegen den HERRN und den von ihm Gesalbten:
3 “Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
»Laßt uns zerreißen ihre Bande und von uns werfen ihre Fesseln!«
4 Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
Der im Himmel thront, der lacht, der Allherr spottet ihrer.
5 Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
Dann aber wird er zu ihnen reden in seinem Zorn und sie schrecken in seinem Ingrimm:
6 “Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
»Habe ich doch meinen König eingesetzt auf dem Zion, meinem heiligen Berge!« –
7 Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
Laßt mich kundtun den Ratschluß des HERRN! Er hat zu mir gesagt: »Mein Sohn bist du; ich selbst habe heute dich gezeugt.
8 Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
Fordre von mir, so gebe ich dir die Völker zum Erbe und dir zum Besitz die Enden der Erde.
9 Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
Du sollst sie mit eiserner Keule zerschmettern, wie Töpfergeschirr sie zerschlagen!« –
10 Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
So nehmt denn Klugheit an, ihr Könige, laßt euch warnen, ihr Richter der Erde!
11 Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
Dienet dem HERRN mit Furcht und jubelt ihm zu mit Zittern!
12 Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.
Küsset den Sohn, auf daß er nicht zürne und ihr zugrunde geht auf eurem Wege! denn leicht entbrennt sein Zorn. Wohl allen, die bei ihm sich bergen!

< Zaburi 2 >