< Zaburi 2 >
1 Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
Why do the heathen rage, And the nations meditate a vain thing?
2 Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
Why do the kings of the earth rise up, And the princes combine together, Against Jehovah, and against his anointed king?
3 “Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
“Let us break their bonds asunder; Let us cast away from us their fetters!”
4 Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
He that sitteth in heaven will laugh; The Lord will have them in derision.
5 Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
Then shall he speak to them in his wrath, And confound them in his hot displeasure.
6 “Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
“I myself have anointed my king, Upon Zion, my holy hill!”
7 Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
I will declare the decree of Jehovah: He hath said to me, “Thou art my son; This day I have begotten thee.
8 Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
Ask of me, and I will give thee the nations for thine inheritance, And the ends of the earth for thy possession.
9 Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
Thou shalt break them with a rod of iron; Thou shalt dash them in pieces like a potter's vessel.”
10 Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
Be wise, therefore, O ye kings! Be admonished, ye rulers of the earth!
11 Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
Be subject to Jehovah with awe, And fear with trembling!
12 Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.
Kiss the son, lest He be angry, and ye perish in your way; For soon shall his wrath be kindled. Happy are all they who seek refuge in him.