< Zaburi 2 >

1 Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
Why have nations assembled tumultuously? And peoples meditate vanity?
2 Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
Kings of the earth station themselves, and princes have been united together, against YHWH, and against His Messiah:
3 “Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
“Let us draw off Their cords, And cast Their thick bands from us.”
4 Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
He who is sitting in the heavens laughs, The Lord mocks at them.
5 Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
Then He speaks to them in His anger, and in His wrath He troubles them:
6 “Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
“And I have anointed My King, On Zion—My holy hill.”
7 Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
I declare concerning a statute: YHWH said to me, “You [are] My Son, today I have brought You forth.
8 Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
Ask of Me and I give nations [as] Your inheritance, And the ends of the earth [for] Your possession.
9 Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
You rule them with a scepter of iron, You crush them as a vessel of a potter.”
10 Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
And now, O kings, act wisely, Be instructed, O judges of earth,
11 Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
Serve YHWH with fear, And rejoice with trembling.
12 Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.
Kiss the Chosen One [[or Son]], lest He is angry, And you perish [from] the way, When His anger burns but a little, O the blessedness of all trusting in Him!

< Zaburi 2 >