< Zaburi 17 >

1 Maombi ya Daudi. Sikia ombi langu kwa ajili ya haki, Yawhe; uusikilize mwito wangu wa msaada. Uyasikilize maombi yangu yatokayo katika midomo isiyo na udanganyifu.
Une prière de David. Écoute, Yahvé, mon juste plaidoyer. Prêtez l'oreille à ma prière qui ne sort pas de lèvres trompeuses.
2 Uthibitisho wangu na uje kutoka uweponi mwako; macho yako na yaone kile kilicho sahihi!
Que ma sentence sorte de ta présence. Que vos yeux regardent l'équité.
3 Kama utaujaribu moyo wangu, kama utakuja kwangu wakati wa usiku, wewe utanitakasa na hautapata mipango yeyote ya uovu; mdomo wangu hautavunja sheria.
Tu as éprouvé mon cœur. Tu m'as rendu visite dans la nuit. Vous m'avez jugé, et n'avez rien trouvé. J'ai résolu que ma bouche ne désobéirait pas.
4 Kama kwa matendo ya binadamu, ni katika neno la midomo yako ya kuwa nimejiepusha na njia za wahalifu.
Quant aux actes des hommes, par la parole de tes lèvres, Je me suis tenu à l'écart des voies de la violence.
5 Mwenendo wangu umeshikila kwa umakini mwenendo wako; miguu yangu haija teleza.
Mes pas se sont attachés à tes sentiers. Mes pieds n'ont pas glissé.
6 Nakuita wewe, kwa kuwa unanijibu, Mungu; geizia sikio lako kwangu na usikilize ninapo ongea.
J'ai fait appel à toi, car tu me répondras, Dieu. Tourne ton oreille vers moi. Écoutez mon discours.
7 Onyesha uaminifu wa agano lako katika namna ya ajabu, wewe uokoaye kwa mkono wa haki yako wale wanao kukimbilia wewe kutoka kwa adui zao.
Montre ta merveilleuse bonté, toi qui sauves de leurs ennemis ceux qui se réfugient par ta droite.
8 Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche katika kivuli cha mbawa zako
Garde-moi comme la prunelle de tes yeux. Cache-moi à l'ombre de tes ailes,
9 kutoka katika uwepo wa waovu ambao wananitusi, adui zangu wanizungukao.
des méchants qui m'oppriment, mes ennemis mortels, qui m'entourent.
10 Wao hawana huruma kwa yeyote; midomo yao huongea kwa majivuno.
Ils ferment leurs cœurs insensibles. Avec leur bouche, ils parlent fièrement.
11 Wao wame zizunguka hatua zangu. Wamekaza macho yao wanishambulie mpaka ardhini.
Ils nous ont maintenant entourés sur nos pas. Ils se sont mis en tête de nous jeter à terre.
12 Wao ni kama mfano wa hasira ya simba mawindoni. Ni kama simba kijana anapotokea mafichoni.
Il est comme un lion qui est avide de sa proie, comme un jeune lion à l'affût dans les endroits secrets.
13 Inuka, Yahwe! Uwashambulie! Uwaangushe chini kwenye nyuso zao! Uyaokoe maisha yangu kutokana na waovu kwa upanga wako!
Lève-toi, Yahvé, confronte-le. Rejetez-le. Délivre mon âme des méchants par ton épée,
14 Uniokoe kutoka kwa watu hawa kwa mkono wako, Yahwe, kutoka kwa watu wa dunia hii ambao utajiri wao ni maisha haya pekee! Wewe utayajaza matumbo ya wale uwathaminio na utajiri; watakuwa na watoto wengi na wataacha utajiri wao kwa watoto wao.
des hommes par ta main, Yahvé, des hommes du monde, dont la part est dans cette vie. Vous remplissez le ventre de ceux que vous aimez. Vos fils en ont plein, et ils accumulent des richesses pour leurs enfants.
15 Bali mimi, nitauona uso wako katika haki; Nitashuhudiwa, pale nitakapo amka, na macho yako.
Quant à moi, je verrai ta face dans la justice. Je me contenterai, à mon réveil, de voir votre forme.

< Zaburi 17 >