< Zaburi 17 >
1 Maombi ya Daudi. Sikia ombi langu kwa ajili ya haki, Yawhe; uusikilize mwito wangu wa msaada. Uyasikilize maombi yangu yatokayo katika midomo isiyo na udanganyifu.
“A psalm of David.” Hear the righteous cause, O LORD! Attend to my cry; Give ear to my prayer from lips without deceit!
2 Uthibitisho wangu na uje kutoka uweponi mwako; macho yako na yaone kile kilicho sahihi!
May my sentence come forth from thy presence; May thine eyes behold uprightness!
3 Kama utaujaribu moyo wangu, kama utakuja kwangu wakati wa usiku, wewe utanitakasa na hautapata mipango yeyote ya uovu; mdomo wangu hautavunja sheria.
Provest thou my heart, visitest thou me in the night, Triest thou me like gold, thou shalt find nothing!
4 Kama kwa matendo ya binadamu, ni katika neno la midomo yako ya kuwa nimejiepusha na njia za wahalifu.
My thoughts do not vary from my lips. As to the deeds of men, Through the word of thy lips I have kept me from the paths of the destroyer.
5 Mwenendo wangu umeshikila kwa umakini mwenendo wako; miguu yangu haija teleza.
Support my steps in thy paths, That my feet may not slip!
6 Nakuita wewe, kwa kuwa unanijibu, Mungu; geizia sikio lako kwangu na usikilize ninapo ongea.
I call upon thee, O God! for thou wilt hear me; Incline thine ear to me, and listen to my prayer!
7 Onyesha uaminifu wa agano lako katika namna ya ajabu, wewe uokoaye kwa mkono wa haki yako wale wanao kukimbilia wewe kutoka kwa adui zao.
Show forth thy loving-kindness, O thou that savest by thy right hand Them that seek refuge in thee from their adversaries!
8 Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche katika kivuli cha mbawa zako
Guard me as the apple of the eye; Hide me under the shadow of thy wings
9 kutoka katika uwepo wa waovu ambao wananitusi, adui zangu wanizungukao.
From the wicked who assault me, From my deadly enemies who compass me about!
10 Wao hawana huruma kwa yeyote; midomo yao huongea kwa majivuno.
They shut up their hard heart; With their mouth they speak haughtily.
11 Wao wame zizunguka hatua zangu. Wamekaza macho yao wanishambulie mpaka ardhini.
They encompass us in all our steps; They fix their eyes upon us, that they may cast us on the ground.
12 Wao ni kama mfano wa hasira ya simba mawindoni. Ni kama simba kijana anapotokea mafichoni.
They are like a lion, eager for his prey; Like a young lion, lurking in secret places.
13 Inuka, Yahwe! Uwashambulie! Uwaangushe chini kwenye nyuso zao! Uyaokoe maisha yangu kutokana na waovu kwa upanga wako!
Arise, O LORD! disappoint them, cast them down! Deliver me from the wicked by thy sword,
14 Uniokoe kutoka kwa watu hawa kwa mkono wako, Yahwe, kutoka kwa watu wa dunia hii ambao utajiri wao ni maisha haya pekee! Wewe utayajaza matumbo ya wale uwathaminio na utajiri; watakuwa na watoto wengi na wataacha utajiri wao kwa watoto wao.
From men, by thy hand, O LORD! from men of the world, Whose portion is in life; whom thou loadest with thy treasure; Whose children have enough, and leave their superfluity to their children.
15 Bali mimi, nitauona uso wako katika haki; Nitashuhudiwa, pale nitakapo amka, na macho yako.
But I through righteousness shall see thy face; I shall be satisfied with the revival of thy countenance.