< Zaburi 17 >
1 Maombi ya Daudi. Sikia ombi langu kwa ajili ya haki, Yawhe; uusikilize mwito wangu wa msaada. Uyasikilize maombi yangu yatokayo katika midomo isiyo na udanganyifu.
“A prayer of David.” Hear, O Lord, [the cause of] righteousness, attend unto my entreaty, give ear unto my prayer, coming from lips without deceit.
2 Uthibitisho wangu na uje kutoka uweponi mwako; macho yako na yaone kile kilicho sahihi!
Let from thy presence my sentence come forth; let thy eyes behold what is right.
3 Kama utaujaribu moyo wangu, kama utakuja kwangu wakati wa usiku, wewe utanitakasa na hautapata mipango yeyote ya uovu; mdomo wangu hautavunja sheria.
Thou hast proved my heart; thou hast thought of me in the night; thou hast refined me—thou couldst find nothing: my purpose doth not pass beyond [the words of] my mouth.
4 Kama kwa matendo ya binadamu, ni katika neno la midomo yako ya kuwa nimejiepusha na njia za wahalifu.
Among the deeds of men did I observe, by the word of thy lips, the paths of the dissolute.
5 Mwenendo wangu umeshikila kwa umakini mwenendo wako; miguu yangu haija teleza.
My steps held firmly to thy tracks, [and] my footsteps did not slip.
6 Nakuita wewe, kwa kuwa unanijibu, Mungu; geizia sikio lako kwangu na usikilize ninapo ongea.
I call on thee, for thou wilt answer me, O God: incline thy ear unto me, hear my speech.
7 Onyesha uaminifu wa agano lako katika namna ya ajabu, wewe uokoaye kwa mkono wa haki yako wale wanao kukimbilia wewe kutoka kwa adui zao.
Show marvelously thy loving-kindnesses, O thou that savest those who put their trust [in thee] from those that rise up [against them] by thy right hand.
8 Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche katika kivuli cha mbawa zako
Keep me as the apple of the eye; conceal me under the shadow of thy wings,
9 kutoka katika uwepo wa waovu ambao wananitusi, adui zangu wanizungukao.
From the wicked that despoil me, my enemies, who, to take my life, compass me about.
10 Wao hawana huruma kwa yeyote; midomo yao huongea kwa majivuno.
They are enclosed in their own fat: with their mouth they speak proudly.
11 Wao wame zizunguka hatua zangu. Wamekaza macho yao wanishambulie mpaka ardhini.
On our steps they now encompass us: they direct their eyes to turn aside in the land.
12 Wao ni kama mfano wa hasira ya simba mawindoni. Ni kama simba kijana anapotokea mafichoni.
Every man is just like a lion that is greedy to tear his prey, and like a young lion lurking in a covert.
13 Inuka, Yahwe! Uwashambulie! Uwaangushe chini kwenye nyuso zao! Uyaokoe maisha yangu kutokana na waovu kwa upanga wako!
Arise, O Lord, prevent him, cast him down; deliver my soul from the wicked, who is thy sword, —
14 Uniokoe kutoka kwa watu hawa kwa mkono wako, Yahwe, kutoka kwa watu wa dunia hii ambao utajiri wao ni maisha haya pekee! Wewe utayajaza matumbo ya wale uwathaminio na utajiri; watakuwa na watoto wengi na wataacha utajiri wao kwa watoto wao.
From these men—thy hand—O Lord, from the men of this world, whose portion is in this life, and whose belly thou fillest with thy hidden treasure: they have children in plenty, and leave the rest of their substance to their babes.
15 Bali mimi, nitauona uso wako katika haki; Nitashuhudiwa, pale nitakapo amka, na macho yako.
As for me, in righteousness shall I behold thy face: I shall be satisfied, when I awake, with contemplating thy likeness.