< Zaburi 16 >

1 Unilinde, Mungu, kwa kuwa nakimbilia kwako kwa ajili ya usalama.
מכתם לדוד שמרני אל כי-חסיתי בך
2 Nami ninasema kwa Yahwe, “Wewe ni Bwana wangu; wema wangu ni bure pasipo wewe.
אמרת ליהוה אדני אתה טובתי בל-עליך
3 Kama kwa watakatifu walioko duniani, ndio walio bora; furaha yangu yote iko kwao.
לקדושים אשר-בארץ המה ואדירי כל-חפצי-בם
4 Taabu yao itaongezeka, wale watafutao miungu mingine. Sitamimina sadaka ya damu kwa miungu yao. Wala kuyainua majina yao kwa midomo yao.
ירבו עצבותם אחר מהרו בל-אסיך נסכיהם מדם ובל-אשא את-שמותם על-שפתי
5 Yahwe, wewe ni sehemu ya chaguo langu na kikombe changu. Unaishikilia kesho yangu.
יהוה מנת-חלקי וכוסי-- אתה תומיך גורלי
6 Mistari iliyo pimwa imelelazwa mahari pa kufurahisha kwa ajili yangu; hakika urithi ufurahishao ni wangu.
חבלים נפלו-לי בנעמים אף-נחלת שפרה עלי
7 Nitakubariki Yahwe, wewe unishauliye; hata wakati wa usiku akili zangu za nielekeza.
אברך--את-יהוה אשר יעצני אף-לילות יסרוני כליותי
8 Nimemuweka Yahwe mbele yangu kila wakati, ili nisitikisike kutoka mkono wake wa kuume.
שויתי יהוה לנגדי תמיד כי מימיני בל-אמוט
9 Kwa hiyo moyo wangu unafuraha, utukufu wangu washangilia. Hakika nitaishi katika usalama.
לכן שמח לבי--ויגל כבודי אף-בשרי ישכן לבטח
10 Kwa kuwa hautaiacha roho yangu kuzimuni. Wewe hautamuacha mwaminifu wako kuliona shimo. (Sheol h7585)
כי לא-תעזב נפשי לשאול לא-תתן חסידך לראות שחת (Sheol h7585)
11 Wewe hunifundisha njia ya maisha; furaha tele inakaa katika uwepo wako; furaha inakaa katika mkono wako wa kuume milele!”
תודיעני ארח חיים שבע שמחות את-פניך נעמות בימינך נצח

< Zaburi 16 >