< Zaburi 150 >
1 Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe katika patakatifu pake; msifuni katika mbingu za ukuu wake.
Alelu-JAH. Alabad a Dios en su santuario; alabadle en el extendimiento de su fortaleza.
2 Msifuni yeye kwa matendo yake makuu; msifuni yeye kwa kadri ya wingi wa ukuu wake.
Alabadle por sus proezas; alabadle conforme a la muchedumbre de su grandeza.
3 Msifuni kwa mlipuko wa pembe; msifuni kwa kinanda na kinubi.
Alabadle a son de shofar; alabadle con salterio y arpa.
4 Msifuni kwa ngoma na kucheza; msifuni kwa vyombo vya nyuzi na filimbi.
Alabadle con adufe y flauta; alabadle con cuerdas y órgano.
5 Msifuni kwa matoazi yavumayo; msifuni kwa matoazi avumayo sana.
Alabadle con címbalos resonantes; alabadle con címbalos de júbilo.
6 Kila kilicho na pumzi kimsifu Yahwe. Msifuni Yahwe.
Todo lo que respira alabe a JAH. Alelu-JAH.