< Zaburi 149 >
1 Msifuni Yahwe. Mwimbieni Yahwe wimbo mpya; imbeni sifa zake katika kusanyiko la waaminifu.
Halleluja. Śpiewajcie Panu pieśń nową; chwała jego niechaj zabrzmi w zgromadzeniu świętych.
2 Israeli ishangilie katika yeye aliye iumba; watu wa Sayuni na washangilie katika mfalme wao.
Wesel się, Izraelu! w Twórcy swoim; synowie Syońscy! radujcie się w królu swoim.
3 Nao walisifu jina lake kwa kucheza; na wamuimbie sifa yeye kwa ngoma na kinubi.
Chwalcie imię jego na piszczałkach; na bębnie i na harfie grajcie mu.
4 Kwa kuwa Yahwe hupata furaha katika watu wake; huwapa utukufu wanyeyekevu kwa wokovu.
Albowiem się kocha Pan w ludu swym; pokornych zbawieniem uwielbia.
5 Wacha Mungu wauchangilie ushindi; nao waimbe kwa furaha vitandani mwao.
Radować się będą święci w chwale Bożej, a śpiewać będą w pokojach swych.
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na panga mbili zenye makali mkononi mwao
Wysławiania Boże będą w ustach ich, a miecz na obie strony ostry w rękach ich,
7 kutekeleza kisasi juu ya mataifa na matendo ya adhabu juu ya watu.
Aby wykonywali pomstę nad poganami, a karali narody;
8 Nao watawafunga wafalme wao kwa minyororo na wakuu wao kwa pingu za chuma. Watatekeleza hukumu ambayo imeandikwa.
Aby wiązali pętami królów ich, a szlachtę ich okowami żelaznemi;
9 Hii itakuwa ni heshima kwa ajili ya watakatifu wake wote. Msifuni Yahwe.
Aby postąpili z nimi według prawa zapisanego. Tać jest sława wszystkich świętych jego. Halleluja.