< Zaburi 149 >

1 Msifuni Yahwe. Mwimbieni Yahwe wimbo mpya; imbeni sifa zake katika kusanyiko la waaminifu.
הַלְלוּ יָהּ ׀ שִׁירוּ לַֽיהוָה שִׁיר חָדָשׁ תְּהִלָּתוֹ בִּקְהַל חֲסִידִֽים׃
2 Israeli ishangilie katika yeye aliye iumba; watu wa Sayuni na washangilie katika mfalme wao.
יִשְׂמַח יִשְׂרָאֵל בְּעֹשָׂיו בְּנֵֽי־צִיּוֹן יָגִילוּ בְמַלְכָּֽם׃
3 Nao walisifu jina lake kwa kucheza; na wamuimbie sifa yeye kwa ngoma na kinubi.
יְהַֽלְלוּ שְׁמוֹ בְמָחוֹל בְּתֹף וְכִנּוֹר יְזַמְּרוּ־לֽוֹ׃
4 Kwa kuwa Yahwe hupata furaha katika watu wake; huwapa utukufu wanyeyekevu kwa wokovu.
כִּֽי־רוֹצֶה יְהוָה בְּעַמּוֹ יְפָאֵר עֲנָוִים בִּישׁוּעָֽה׃
5 Wacha Mungu wauchangilie ushindi; nao waimbe kwa furaha vitandani mwao.
יַעְלְזוּ חֲסִידִים בְּכָבוֹד יְרַנְּנוּ עַל־מִשְׁכְּבוֹתָֽם׃
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na panga mbili zenye makali mkononi mwao
רוֹמְמוֹת אֵל בִּגְרוֹנָם וְחֶרֶב פִּֽיפִיּוֹת בְּיָדָֽם׃
7 kutekeleza kisasi juu ya mataifa na matendo ya adhabu juu ya watu.
לַעֲשׂוֹת נְקָמָה בַּגּוֹיִם תּֽוֹכֵחֹת בַּל־אֻמִּֽים׃
8 Nao watawafunga wafalme wao kwa minyororo na wakuu wao kwa pingu za chuma. Watatekeleza hukumu ambayo imeandikwa.
לֶאְסֹר מַלְכֵיהֶם בְּזִקִּים וְנִכְבְּדֵיהֶם בְּכַבְלֵי בַרְזֶֽל׃
9 Hii itakuwa ni heshima kwa ajili ya watakatifu wake wote. Msifuni Yahwe.
לַעֲשׂוֹת בָּהֶם ׀ מִשְׁפָּט כָּתוּב הָדָר הוּא לְכָל־חֲסִידָיו הַֽלְלוּ־יָֽהּ׃

< Zaburi 149 >