< Zaburi 148 >
1 Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
Alaba al Señor Que el Señor sea alabado desde los cielos; dele gracias en los cielos.
2 Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
Alábenle, todos sus ángeles: alabenle, todos sus ejércitos.
3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
Alábenlo. sol y luna: alábenle. todas las estrellas de luz.
4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
Alábenle, cielos más altos, y aguas que están sobre los cielos.
5 Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
Alaben el nombre de Jehová; porque él dio la orden, y fueron hechos.
6 Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
El los ha puesto en su lugar para siempre; él les ha dado sus límites que no pueden romperse.
7 Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
Alaben al Señor desde la tierra, grandes animales de mar y lugares profundos.
8 moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
Fuego y lluvia de hielo, nieve y neblinas; Tormenta de viento, ejecutan su palabra:
9 Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
Montañas y todas las colinas; árboles frutales y todos los árboles de las montañas:
10 wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
Bestias y todo ganado; insectos y pájaros alados:
11 Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
Reyes de la tierra y todos los pueblos; gobernantes y todos los jueces de la tierra:
12 wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
jóvenes y vírgenes; ancianos y niños:
13 Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
Dejen que glorifiquen el nombre del Señor; porque sólo su nombre es alabado: su reino está sobre la tierra y el cielo.
14 Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.
Alzó el poderío de su pueblo para alabanza de todos sus santos; incluso los hijos de Israel, un pueblo que está cerca de él. que el Señor sea alabado.