< Zaburi 148 >
1 Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
Alleluia. Lodate l’Eterno dai cieli, lodatelo nei luoghi altissimi.
2 Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
Lodatelo, voi tutti gli angeli suoi, lodatelo, voi tutti i suoi eserciti!
3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
Lodatelo, sole e luna, lodatelo voi tutte, stelle lucenti!
4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
Lodatelo, cieli dei cieli, e voi acque al disopra dei cieli!
5 Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
Tutte queste cose lodino il nome dell’Eterno, perch’egli comandò, e furon create;
6 Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
ed egli le ha stabilite in sempiterno; ha dato loro una legge che non trapasserà.
7 Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
Lodate l’Eterno dalla terra, voi mostri marini e abissi tutti,
8 moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
fuoco e gragnuola, neve e vapori, vento impetuoso che eseguisci la sua parola;
9 Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
monti e colli tutti, alberi fruttiferi e cedri tutti;
10 wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
fiere e tutto il bestiame, rettili e uccelli alati;
11 Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
re della terra e popoli tutti principi e tutti, i giudici della terra;
12 wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
giovani ed anche fanciulle, vecchi e bambini!
13 Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
Lodino il nome dell’Eterno; perché il nome suo solo è esaltato; la sua maestà è al disopra della terra e del cielo.
14 Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.
Egli ha ridato forza al suo popolo, dando motivo di lode a tutti i suoi fedeli, ai figliuoli d’Israele, al popolo che gli sta vicino. Alleluia.