< Zaburi 148 >

1 Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
Louez l'Eternel. Louez des cieux l'Eternel; louez-le dans les hauts lieux.
2 Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
Tous ses Anges, louez-le; toutes ses armées, louez-le.
3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
Louez-le, vous soleil et lune; toutes les étoiles qui jetez de la lumière, louez-le.
4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
Louez-le, vous cieux des cieux; et [vous] eaux qui êtes sur les cieux.
5 Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
Que ces choses louent le Nom de l’Eternel; car il a commandé, et elles ont été créées.
6 Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
Et il les a établies à perpétuité [et] à toujours; il y a mis une ordonnance qui ne passera point.
7 Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
Louez de la terre l'Eternel; [louez-le], baleines, et tous les abîmes,
8 moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
Feu et grêle, neige, et vapeur, vent de tourbillon, qui exécutez sa parole,
9 Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
Montagnes, et tous coteaux, arbres fruitiers, et tous cèdres,
10 wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
Bêtes sauvages, et tout bétail, reptiles, et oiseaux qui avez des ailes,
11 Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
Rois de la terre, et tous peuples, Princes, et tous Gouverneurs de la terre.
12 wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
Ceux qui sont à la fleur de leur âge, et les vierges aussi, les vieillards, et les jeunes gens.
13 Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
Qu'ils louent le Nom de l’Eternel; car son Nom seul est haut élevé; sa Majesté est sur la terre, [et] sur les cieux.
14 Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.
Et il a fait lever en haut une corne à son peuple, [ce qui est] une louange à tous ses bien-aimés, aux enfants d'Israël, qui est le peuple qui est près de lui. Louez l'Eternel.

< Zaburi 148 >