< Zaburi 148 >

1 Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
Alléluia! Louez l’Eternel dans les sphères célestes, louez-le dans les régions supérieures!
2 Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
Louez-le, vous tous, ses anges, louez-le, vous, ses milices,
3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
louez-le, vous, soleil et lune, louez-le, vous toutes, étoiles lumineuses.
4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
Louez-le, cieux des cieux, et vous, eaux supérieures, au-dessus des cieux.
5 Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
Que tous les êtres louent le nom de l’Eternel, car il a ordonné, et ils furent créés.
6 Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
Il les maintient jusque dans l’éternité, il leur a tracé des lois qui sont immuables.
7 Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
Louez l’Eternel sur toute l’étendue de la terre: monstres marins et vagues profondes,
8 moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
foudre et grêle, neige et brouillard, vent de tempête, chargé d’exécuter ses ordres,
9 Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
montagnes et collines, toutes ensemble, arbres fruitiers et cèdres réunis,
10 wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
bêtes sauvages et animaux domestiques, reptiles, oiseaux ailés,
11 Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
rois de la terre et vous tous, ô peuples, princes et juges de la terre,
12 wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
jeunes gens et vierges, vieillards de concert avec les adolescents!
13 Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
Célébrez le nom de l’Eternel, car seul son nom est sublime; sa splendeur s’étend sur la terre et dans les cieux.
14 Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.
Il a grandi la force de son peuple; aussi est-il l’objet des louanges de tous ses pieux adorateurs, des enfants d’Israël, du peuple qu’il a rapproché de lui. Alléluia!

< Zaburi 148 >