< Zaburi 148 >

1 Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
Praise ye the LORD. Praise ye the LORD from the heavens: praise him in the hights.
2 Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
Praise ye him, all his angels: praise ye him, all his hosts.
3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
Praise ye him, sun and moon: praise him, all ye stars of light.
4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
Praise him, ye heavens of heavens, and ye waters that [are] above the heavens.
5 Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
Let them praise the name of the LORD: for he commanded, and they were created.
6 Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
He hath also established them for ever and ever: he hath made a decree which shall not pass.
7 Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
Praise the LORD from the earth, ye dragons, and all deeps:
8 moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
Fire, and hail; snow, and vapors; stormy wind fulfilling his word:
9 Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
Mountains, and all hills; fruitful trees, and all cedars:
10 wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
Beasts, and all cattle; creeping animals, and flying fowl:
11 Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
Kings of the earth, and all people; princes, and all judges of the earth:
12 wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
Both young men, and maidens; old men, and children:
13 Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
Let them praise the name of the LORD: for his name alone is excellent; his glory [is] above the earth and heaven.
14 Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.
He also exalteth the horn of his people, the praise of all his saints; [even] of the children of Israel, a people near to him. Praise ye the LORD.

< Zaburi 148 >