< Zaburi 148 >

1 Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
Praise Yahweh! Praise him, from up in heaven; praise him from way up in the sky!
2 Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
All you angels who belong to him, praise him! All you who are in the armies of heaven, praise him!
3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
Sun and moon, [you also] praise him! You shining stars, you praise him!
4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
You highest heavens, praise him! And you waters that are high above the sky, praise him!
5 Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
I want [all of] these to praise Yahweh [MTY] because by commanding [them to exist], he created them.
6 Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
He determined the places where they should be [in the sky], and he commanded that they should be there forever. They cannot disobey that command!
7 Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
And everything on the earth, praise Yahweh! You [huge] sea monsters and [everything else that is] deep [in the ocean],
8 moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
and fire and hail, and snow and frost, and strong winds that obey what he commands, [I tell] all of you to praise Yahweh!
9 Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
Hills and mountains, fruit trees and cedar [trees],
10 wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
all the wild animals and all [you] cattle, and the (reptiles/creatures that scurry across the ground), and [all] the birds, [I tell all of them to praise Yahweh]!
11 Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
You kings on this earth and all the people [that you rule], you princes and all [other] rulers,
12 wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
you young men and young women, you old people and children, [everyone, praise Yahweh!]
13 Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
I want them [all] to praise Yahweh [MTY] because he is greater than anyone else. His glory is greater than [anything on] the earth or [in] heaven.
14 Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.
He caused us, his people, to be strong in order that we, his people, we Israeli people (who are very precious to him/whom he loves very much), would praise him. So praise Yahweh!

< Zaburi 148 >