< Zaburi 148 >
1 Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
Alleluia, [a Psalm] of Aggaeus and Zacharias. Praise you the Lord from the heavens: praise him in the highest.
2 Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
Praise you him, all his angels: praise you him, all his hosts.
3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
Praise him, sun and moon; praise him, all you stars and light.
4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
Praise him, you heavens of heavens, and the water that is above the heavens.
5 Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
Let them praise the name of the Lord: for he spoke, and they were made; he commanded, and they were created.
6 Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
He has established them for ever, even for ever and ever: he has made an ordinance, and it shall not pass away.
7 Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
Praise the Lord from the earth, you serpents, and all deeps.
8 moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
Fire, hail, snow, ice, stormy wind; the things that perform his word.
9 Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
Mountains, and all hills; fruitful trees, and all cedars:
10 wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
wild beasts, and all cattle; reptiles, and winged birds:
11 Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
kings of the earth, and all peoples; princes, and all judges of the earth:
12 wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
young men and virgins, old men with youths:
13 Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
let them praise the name of the Lord: for his name only is exalted; his praise is above the earth and heaven,
14 Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.
and he shall exalt the horn of his people, [there is] a hymn for all his saints, [even] of the children of Israel, a people who draw near to him.