< Zaburi 146 >
1 Msifu Yahwe. Msifu Yahwe, ee nafsi yangu.
Alleluja, Aggæi et Zachariæ.
2 Ninamsifu Mungu maisha yangu yote; nitamuimbia sifa Mungu wangu ni ngali ni hai.
Lauda, anima mea, Dominum. Laudabo Dominum in vita mea; psallam Deo meo quamdiu fuero. Nolite confidere in principibus,
3 Msiweke imani katika wakuu au wanadamu, ambaye katika yeye hamna wokovu.
in filiis hominum, in quibus non est salus.
4 Wakati uhai wa pumzi ya mtu unapokoma, hurudi aridhini; siku hiyo mipango yake hufikia mwisho.
Exibit spiritus ejus, et revertetur in terram suam; in illa die peribunt omnes cogitationes eorum.
5 Amebarikiwa yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yahwe Mungu wake.
Beatus cujus Deus Jacob adjutor ejus, spes ejus in Domino Deo ipsius:
6 Yahwe aliumba mbingu na nchi, bahari, na vyote vilivyomo; huitazama kweli milele.
qui fecit cælum et terram, mare, et omnia quæ in eis sunt.
7 Yeye hutekeleza hukumu kwa ajili ya walioonewa na huwapa chakula wenye njaa. Yahwe huwafungua waliofungwa;
Qui custodit veritatem in sæculum; facit judicium injuriam patientibus; dat escam esurientibus. Dominus solvit compeditos;
8 Yahwe huyafungua macho ya kipofu; Yahwe huwainua walioinama; Yahwe huwapenda watu wenye haki.
Dominus illuminat cæcos. Dominus erigit elisos; Dominus diligit justos.
9 Yahwe huwalinda wageni katika nchi; huwainua yatima na wajane, bali huipinga njia ya wasio haki.
Dominus custodit advenas, pupillum et viduam suscipiet, et vias peccatorum disperdet.
10 Yahwe atatawala milele, Mungu wako, Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Yahwe.
Regnabit Dominus in sæcula; Deus tuus, Sion, in generationem et generationem.